Miili ya waliofariki ikishushwa Toka katika magari tayari Kwa kuagwa na wakazi wa Arusha |
Na :Andrea Ngobole, MAIPAC
maipacarusha20@gmail.com
Miili ya watu 25 waliofariki kwa ajali iliyohisisha Lori lililobea mtambo wa kuchongea barabara na magari mengine matatu, inaagwa Leo February 27 katika Uwanja wa Sheikh Amri Abeid jijini Arusha.
Ajali hiyo ilitokea February 24 majira ya jioni eneo la Ngaramtoni kibaoni Bypass Wilaya ya Arumeru Mkoani Arusha.
Mkuu wa Mkoa wa Arusha John Mongela atakayeongoza wakazi wa Mkoa wa Arusha kuaga miili hiyo amesema kuwepo Kwa Zoezi Hilo hakuwezi kuathiri maandamano ya Chadema yanayofanyika mkoani Arusha leo kwani Serikali inatambua maandamano hayo.
"Naomba isije ikapotoshwa si kwamba hatutambui uwepo wa maandamano, ratiba ya maandamano IPO na IPO kisheriana mifumo yote ya Serikali itahakikisha maandamano haya yanakuwa salama kama yalivuosimamiwa Maneno mengine" alisema Mongela
Kwa mujibu wa ratiba iliyotolewa na ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Arusha shughuli za kuaga miili hiyo itaanza saa tatu asubuhi na kukamilika saa Tano Kisha miili hiyo kusafirishwa maeneo mbalimbali Kwa ajili ya maziko
No comments:
Post a Comment