Mwandishi Wetu, Moscow
maipacarusha20@gmail.com
RAIS Dkt. Samia Suluhu Hassan ameitoa shahada ya heshima ya uzamivu aliyotunukiwa nchini Urusi kwa wanafunzi, wazazi na walimu wanaopambana kuboresha maendeleo ya nchi kwa kutumia elimu.
Akizungumza mara baada ya kutunukiwa shahada hiyo ya honoris causa, Rais Samia amesema ameipokea tuzo hiyo kwa unyenyekevu mkubwa lakini anaamini ni kwa niaba ya wengi wengine.
kutokana na uongozi usio kifani na mchango wake kwa maendeleo ya taifa lake.
Chuo Kikuu cha Urafiki wa Watu wa Urusi (RUDN) cha Patrick Lumumba kimempa Rais Samia heshima hiyo kwa sababu ya uongozi uliotukuka na jitihada zake za kuiletea Tanzania maendeleo.
Nilipopata taarifa ya kupewa hadhi hii, niliona kwamba hii heshima si yangu pekee bali ni kwa wale wote ambao elimu ina maana kwao. Kwa walimu wanaofundisha kote, kwa wanafunzi want guys maarifa na kwa wazazi wanaopambana kusomesha watoto wao.
“ Jina la chuo hiki, likichukua jina la mmoja wa viongozi wanamapinduzi wa Afrika la Patrice Lumumba ni kielelezo cha ushahidi wa uhusiano unaojali ukombozi, utu na umoja wa kweli,” alisema.
RUDN ni miongoni mwa vyuo mashuhuri duniani – kikijipatia sifa kutokana na kusomesha kada ya wasomi wa miaka ya mwanzoni ya Uhuru barani Afrika, Asia na Amerika ya Kusini na kujulikana kwa jina la Patrice Lumumba.
Shahada hiyo ya heshima ya RUDN ni ya nane kwa Rais Samia tangu aingie madarakani mwaka 2021.


No comments:
Post a Comment