Sungura wakiwa katika Banda maalum ambalo hufugwa ili kukusanya mkojo. |
Mwandishi wetu, Maipac
maipacarusha20@gmail.com
Changamoto za matumizi ya mbolea na madawa ya kilimo ya viwandani,kumeibua biashara mpya ambayo inakuwa kwa kasi nchini.
Biashara
hiyo ni ya mkojo wa sungura ambao unauzwa kwa lita kati ya sh 7000 hadi
10,000 bei kubwa kupita hata bei ya mafuta ya petroli.
Wateja wakubwa wa mkojo huu ni wakulima wa maeneo ya mkoa wa Arusha na Kilimanjaro,Mbeya,Njombe, Songwe na mikoa mingine ambayo inalima mboga mboga na matunda.
Lakini soko hili pia limeibua biashara ya ufugaji sungura katika mashamba makubwa na kuwa na sungura kati ya 5000 hadi 10,000.
Mkojo
wa sungura umethibitishwa na wataalamu wa kilimo kama dawa la kufukuza
wadudu shambani ,kupata mbolea na kuimarisha afya ya mimea.
Mahitaji
ya mkojo huo, yamekuwa yakiongezeka siku hadi siku, hasa kutokana na
kuthibitika una uwezo mkubwa wa kufukuza wadudu waharibifu shambani
lakini pia kuimarisha afya ya mmea.
Uchunguzi
uliofanywa katika baadhi ya mashamba ya kilimo Hai,(kilimo
ambacho hakitumii mbolea za viwandani na pembejeo za viwandani)
umebaini kwa sasa kuna ongeko la mahitaji ya mkojo wa sungura kwa
wakulima na kumesababisha bei yake kupaa kutoka kiasi cha sh 2000 kwa
lita hadi kati ya sh 7000 hadi 10000.
Lita
moja na nusu ya mkojo wa sungura inachanganywa na lita 10 za maji na
baada ya kuchanganya huweza kupulizia shamba hadi hekali moja kulingana
na mazao yaliyopo shambani.
Mtaalam wa ufugaji Sungura katika shamba la kiogani la St Joseph lilipo Kwanyange Wilaya Mwanga Mkoa Kilimanjaro, Felisian Pius anasema matumizi ya mkojo wa Sungura imekuwa ni suluhu kwa wakulima ,kudhibiti wadudu waharibifu na kuimarisha afya ya mimea.
Anasema
matumizi hayo ya mkojo wa Sungura yamevutia watu wengi kujikita pia
katika ufugaji wa sungura ili kuvuna mkojo huo kwa matumizi ya
mashambani na kwenye bustani.
Dr.Peter
Mushi mtaalamu wa dawa za kilimo na mifugo anasema kitaalamu
imethibitika mkojo wa sungura una kemikali ambazo zinaua wadudu lakini
hazina athari kwa binadamu.
"Bado
tafiti zaidi zinaendelea duniani kuhusiana na mkojo wa sungura huenda
miaka ijayo ukaboreshwa na kuuzwa kitalaamu wa zaidi"amesema
Mtaalam wa ufugaji sungura na kutengeneza dawa ya kuuwa wadudu na kuimarisha mmea Felisian Pius katika shamba la kiogan la st Joseph kwanyange Mwanga akionesha jinsi ya kukusanya mkojo |
Jinsi ya kuwandaa Sungura hadi kuvuna mkono wao.
Pius
anasema Sungura wanapaswa kufugwa katika mabanda maalum ambayo ni
rahisi kukusanya mkono wao na kupewa chakula cha kutosha hasa majani
yenye ukavu na maji kwa wingi.
Anasema
Sungura wanapaswa kujengewa banda la mabanzi na kuishi juu na
kuhakikisha sungura wa familia moja hawazaliani ili kuepuka magonjwa na
vifo.
Anasema Sungura
watano hadi kumi walioshiba vizuri na kupewa maji ya kutosha wanaweza
kuzalisha mkono wa kutosha kwa ajili ya shamba na bustani kwa mwaka
mzima na kwa siku wanaweza kuzalisha lita moja ya mkojo.
Anasema
mkojo unaweza kukusanywa kupitia mfumo wa kuwa na sehemu ya kukusanya
mkojo kupitia boma maalum, ambao sio rahisi kuharibika ama kumwagika.
Mkojo
huo wa Sungura ukiwa unakusanywa kwenye bomba hilo ambalo unaweza
kuliweka nyuma ya Banda lililojegwa kwa kuliweka upande mmoja
umeinuka kidogo na upande mwngine unakuwa chini.
"boma hilo litasaidia mkojo uweze kutiririka kwa urahisi na kuingia katika chombo maalumu ambacho utakuwa umeandaa"anasema
Anasema
Mfugaji anatakiwa kukusanya mkojo wa sungura mara mbili mpaka Mara tatu
kwa siku ili kuzuia kuchanganyika na maji ikiwepo ya mvua kama
ikinyesha.
Jinsi ya kutumia Mkojo.
Mkojo
wa Sungura ukikusanywa lita moja na nusu na kuchanganywa na lita 10
za maji na mkulima atapuliza katika shamba la ekari moja.
Mkojo
huo unatumika kama Dawa ya kufukuzia wadudu na mbolea ya kurutubisha
mimea Katika shamba lako lenye mchanganyiko wa mimea.
"Jambo
la kuzingatia Katika utiaji wa mkojo wa sungura katika shamba la
mkulima ni kuhakikisha anaweka kwa kila shina kwa chinina sio kuweka
katika majani ya mmea.
Anasema
muda mzuri ya kupuliza dawa hiyo na mkojo wa sungura ni asubuhi kabla
ya jua kuwa kali kwani ikipuliziwa mchana jua likiwa kali mimea inaweza
kuungua.
Faida zitokanazo na matumizi ya mkojo wa sungura.
Mkulima anayetumia mkojo mavuno uongezeka kwa wingi,shamba halitakuwa halina wadudu waharibifu wa mimea.
anasema mkojo huo wasungura kwa kuchanganya na maji pia inasaidia shamba kuwa na rutuba ya kutosha na ulinzi wa udongo.
Mkulima
Leokadia Peter wa kijiji cha kwanyange wilaya ya mwanga mkoa wa
Kilimanjaro anasema tangu aanze kutumia mkojo wa Sungura ameweza
kuimarisha afya ya mimea shambani kwake.
Leokadia
anaeleza amefanikiwa sana katika kilimo cha mbogamboga mara tu
alipoanza kutumia mkojo wa sungura na kubadili hali ya uvunaji kwani
amekuwa akipata mazao mengi hasa mbogamboga ambazo awali zilikuwa
zikisumbuliwa kwa kuliwa na wadudu.
Julius Kanangira ni mkulima wa mbogamboga anasema, tangu ameanza kutumia mbolea zaasili na mkojo wa sungura mavuno yameongezeka.
"mimi situmii mbolea za viwandani, natumia kinyesi cha ng'ombe na mkojo wa sungura tu na nalima mbogamboga kwa ufasini "anasema
Hata hivyo anasema changamoto kubwa ni upatikanaji wa mkojo wa kutosha wa sungura wakati wote.
"nafikiria na mimi kuanza kufuga sungura ili iwe rahisi kupata mkojo na mbolea nyingine"anasema
Akizungumza
na mwananchi,Meneja wa mradi wa mkulima mbunifu Erica Rugabandana
anasema matumizi ya mbolea za asili na mkojo wa Sungura ni suluhisho na
kuacha matumizi ya mbolea na viwandani na madawa kwa ajili ya kukuza
mazao na kupambana na wadudu.
"sisi
tumekuwa na mradi huu ambao ni kilimo endelevu unafadhiliwa na shirika
la biovision (BV) foundation lilipo switzerland na tunaona mafanikio
makubwa kwa wakulima wa kilimo hai"anasema
Mtaalam wa ufugaji sungura na kutengeneza dawa ya kuuwa wadudu na kuimarisha mmea Felisian Pius katika shamba la kiogan la st Joseph kwanyange Mwanga akionesha jinsi ya kukusanya mkojo |
Mratibu
wa programu ya mawasiliano ya shirika la Biovision Afrika
Trust,Fredrick Ochieng anasema kumekuwepo na ongezeko la matumizi ya
pembejeo na mbolea za viwadani ambazo baadhi huzalisha sumu ambayo
inaathiri afya za watu.
"kwa
wakulima kurejea katika kilimo cha asili kwa kutumia mbolea za asili na
pembejeoza asili ni suluhu kubwa katika kupata vyakula salama"anasema
Wengi
hufuga Sungura kwa ajili ya matumizi ya chakula na urembo lakini sasa
Sungura ni dili kwa wakulima hasa baada ya kuthibitika mkojo wake ni
dawa ya kufukuza wadudu lakini pia ni mbolea katika mimea na kurutubisha
ardhi.
No comments:
Post a Comment