Walimu 500 wilaya Karatu wajitoa chama Cha walimu (CWT), baraza la madiwani laridhia - MAIPAC MEDIA TANZANIA

Breaking

MAIPAC MEDIA TANZANIA

A Centre for Indigenous and Pastoralists Community Informations




Saturday 12 August 2023

Walimu 500 wilaya Karatu wajitoa chama Cha walimu (CWT), baraza la madiwani laridhia

 

Baadhi ya walimu wilayani Karatu waliojitoa CWT

Baraza la madiwani halmashauri ya wilaya Karatu 

NA: SOPHIA FUNDI KARATU.


maipacarusha20@gmail.com


Madiwani halmashauri ya wilaya ya KARATU mkoani Arusha wameridhia kwa pamoja ombi la waalimu zaidi ya 500 ya kutokatwa mishahara yao na kilichokuwa chama    Cha waalimu CWT baada ya waalimu hao kujitoa na chama hicho na kujiunga na chama kipya CHAKUHAWATA.


Ombi Hilo   limewasilishwa  na katibu msaidizi wa chama hicho bw  Deogratius Mmao akifuatana na baadhi ya wanachama wa chama hicho ambao walilaani kitendo Cha  idara ya utumushi  kuendelea kukata mishahara yao nakuelekeza CWT Jambo ambalo litaleta mgogoro baina yao.


Madiwani hao wakichangia hoja kwa pamoja waliunga mkono hoja na kumtaka mkurugenzi mtendaji wa halmashauri hiyo Juma Hokororo kupitia idara ya utumishi kuheshimu hoja ya waalimu hao na kuacha kuwakata mishahara  yao nakuelekeza CWT badala yake waelekeze kwenye chama kipya.


Walimwagiza mkurugenzi mtendaji bw Hokororo  kupitia idara ya utumishi kuanzia mwezi huu wa  nane 2023 kuhakikisha hakuna mshahara wa mwalimu unaokatwa na chama hicho ili kuheshimu uhuru wa mwalimu  na kuepuka migogoro baina ya halmashauri na waalimu.


"Mkurugenzi tunakuagiza hakikisha hakuna mshahara wa mwaalimu unaokatwa na chama hicho kuanzia mwezi huu wa nane ni uhuru wa mwalimu kujiunga na chama anachokipenda tuwaache wachague wenyewe tusiwalazimishe, hatutaki kuingia kwenye migogoro na waalimu" alisema John Lucian.


Akizungumza na wanahabari kaimu katibu wa chama hicho Mmao alisema kuwa waalimu hao wamefuata taratibu zote za utumishi na kujiunga na chama hicho kipya CHAKUHAWATA.


Kwa upande wake Mwenyekiti msaidizi wa CHAKUHAWATA bw Festo Mbilinyi ameshukuru Baraza la madiwani kwa kupokea ombi lao  na kukubaliwa ambapo aliomba  mchakato huo uharakishwe ili  uweze kuingia kwenye utekelezaji.

No comments:

Post a Comment