Wadau wa uhifadhi wajadili matumizi ya Teknolojia za kisasa katika uhifadhi wanyamapori - MAIPAC MEDIA TANZANIA

Breaking

MAIPAC MEDIA TANZANIA

A Centre for Indigenous and Pastoralists Community Informations




Saturday 2 March 2024

Wadau wa uhifadhi wajadili matumizi ya Teknolojia za kisasa katika uhifadhi wanyamapori

 





Mussa Juma, Maipac


maipacarusha20@gmail.com


Watafiti na Wahifadhi nchini  wanakutana  kwa siku mbili jijini Arusha kwa lengo la kujadili matumizi ya Technolojia za kisasa katika uhifadhi na mikakati ya pamoja  ya kuimarisha uhifadhi  na  kukuza  utalii  nchini .


Mkutano wa watafiti na wadau wa uhifadhi ni sehemu ya maadhimisho ya  Siku ya Wanyamapori Duniani ambayo huadhimishwa   Machi 03 kila mwaka.

Kaimu Mkurugenzi wa ldara ya Wanyamapori nchini Dk Fourtunata Msoffe


Akifungua mkutano huo  ambao umeratibiwa na Wizara ya Maliasili na Utalii, Kaimu Mkurugenzi Idara ya Wanyamapori Dk. Fortunata Msoffe amesemakuwa  wakati Taifa likiwa kwenye maombelezo ya kifo cha

aliyekuwa Rais wa awamu ya pili  hayati Alli Hassan Mwinyi ni muhimu kwa wahifadhi  na watanzania kwa ujumla  kuenzi jitihada za viongozi katika kutunza Maliasili ya Wanyamapori.


Dkt. Msoffe amesema  hayati Mzee Mwinyi amekuwa na mchango mkubwa kwenye uhifadhi wa rasilimali za wanyapori.


" Kuanzia awamu ya kwanza ya baba wa Taifa hadi sasa ambapo Rais  Dkt. Samia Suluhu Hassan  viongozi wetu wamekuwa wahifadhi namba moja  nchini wenye maono makubwa kwenye Uhifadhi wa raslimali na kukuza Utalii nchini.


"Hapa naomba nisisitize kuwa wamefanya  jitihada  kubwa kuhakikisha Maliasili  inakuwepo kwa kizazi  kilichopita, kilichopo na kijacho ili ziendelee kunufaisha Taifaletu" alisema Dk Msofe .


Mkutano huu unafanyika wakati Wizara ya Maliasili na Utalii ikiwa katika mkakati mkubwa wa kukuza Utalii lakini pia kukabiliana na changamoto za uhifadhi.


Miongoni mwa changamoto hizo ni pamoja na ongezeko la migogoro baina ya wanyamapori na Binaadamu lakini pia uvamizi maeneo ya Mapito ya Wanyamapori (Shoroba)


Waziri wa Maliasili na Utalii, Angellah Kairuki tayari ametangaza mkakati wa kuyapima na kuyalinda maeneo 20 ya Shoroba nchini ili kuendeleza uhifadhi.


Miongoni mwa maeneo hayo ni Shoroba ya Kwakuchinja ambayo ipo katika eneo la Ikolojia la Tarangire -Manyara.


Mkutano huo umejumuisha Watafiti  na Wahifadhi kutoka Idara za Wanyamapori, Misitu na Malikale,  Taasisi  ya  Utafiti  wa  Wanyamapori  Tanzania (TAWIRI), Shirika  la Hifadhi za Taifa (TANAPA), 



Washiriki  wengine ni Mamlaka ya Uhifadhi  Ngorongoro (NCAA), Mamlaka  ya Uhifadhi  wa  Wanyamapori (TAWA), Wakala  wa huduma  za Misitu (TFS), Chuo cha Wanyamapori Mweka na wadau kutoka taasisi zisizo za kiserikali za WWF, FZS, CWMAC, Nature Tanzania, TNRF na AWF.


Katika maadhimisho ya mwaka huu. Kaulimbiu ni‘ *"UNGANISHA WATU NA ULIMWENGU: VUMBUA MATUMIZI YA TEKNOLOJIA YA KIDIGITALI KATIKA UHIFADHI WA WANYAMAPORI"*


Katika mkutano huo pia taarifa mbalimbali za tafiti zinatarajiwa kutolewa katika kuimarisha uhifadhi nchini.


No comments: