MALIMA AAGIZA HALMASHAURI YA MLIMBA KULIMA MAZAO YA MIKAKATI. - MAIPAC MEDIA TANZANIA

Breaking

MAIPAC MEDIA TANZANIA

A Centre for Indigenous and Pastoralists Community Informations




Saturday 22 June 2024

MALIMA AAGIZA HALMASHAURI YA MLIMBA KULIMA MAZAO YA MIKAKATI.

 

MKUU wa Mkoa wa Morogoro, Adam Malima




Na Lilian Kasenene, Morogoro 

maipacarusha20@gmail.com


MKUU wa Mkoa wa Morogoro, Adam Malima amewataka madiwani na watendaji wa Halmashauri ya Mlimba, Wilayani Kilombero,mkoa wa Morogoro kufanya kazi za kuletea maendeleo kwa wananchi na kuhamasisha shughuli za uzalishaji wa mazao ya  kimkakati yatakayochangia kuongeza mapato yao na ya halmashauri kwa ajili ya kuboresha  huduma za kijamii.


Hatua hiyo inatokana na wakulima wa zao la kokoa katika Halmashauri hiyo kuanza  kufaidika  baada ya kufanyika mnada wa kwanza wa ununuzi wa kwa njia ya mtandao uliowaingizia fedha kiasi cha  Shilingi bilioni 1.1.


Katika mnada huo jumla ya kilo 43,750 za Kakao ziliuzwa  kwa bei ya Sh  25,720 kwa kilo, kupitia mfumo wa stakabadhi ghalani unaoratibiwa na Soko la Bidhaa Tanzania (TMX).


Malima alisema hayo wakati wa kikao cha Baraza la Madiwani kujadili hoja sita za Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) kilichofanyika jana  kwenye ukumbi wa mikutano wa halmshauri hiyo .


Alisema halmshauri ya Mlimba kimsingi ni ya kilimo na mapato yake yanategemea mazao ya kilimo yaliwemo ya mpunga, ndizi na kokoa hivyo madiwani na watendaji wanaowajibu kusimamia Maendeleo.


“ Bahati nzuri wiki iliyopita nilikuwa Mlimba na kulikuwa na mnada wa zao kakao uliokusanya tani 43 na zikapatikana Sh bilioni 1.1 na katika hilo fedha iliyoenda halmashauri ni Sh milioni 33” alisema Malima .


Malima alisema , halmashauri hiyo ya Mlimba kutokana na kuwepo  ardhi yenye rubuta na inayofaa kwa kilimo cha mazao mbalimbali yakiwemo ya kimkakati ambayo inauwezo wa kuongoza kimapato kimkoa na kuchangia  kuongeza kipato cha mwananchi na pia kwa halmashauri .


Alisema kuwa ,madiwani kwa kushirikiana na watendaji  wa halmashauri hiyo wakiweka mkazo  kuhamashisha uzalishaji wa zao la kokoa  kwa hatua za awali itaweza kuzalisha tani 1,000  kwa mwaka  zenye thamani ya Sh bilioni 900 na halmashauri kujipati mapato ya zaidi ya Sh bilioni 4 endapo  juhudi hizo zitaongezwa  upo uwezekano wa  kufikia zaidi ya  tani 5,000 wa mwaka.


" Halmashauri hii ya Mlimba inaweza kujiendesha Kwa kokoa tu endapo uzalishaji ukaongezeka mara dufu" alisema Malima.


Mkuu wa mkoa pia aliwatahadharisha  madiwani wanaopingana na Ilani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) kuhusu matumizi ya mfumo wa Stakabadhi Gharani ya  wanajiweka katika  mazingira  magumu.


“Diwani lazima  muwe na wivu wa  maendeleo , Diwani ujiulize mimi ni diwani maendeleo  au diwani maslahi nah ii pia kwa watendaji  mjiuliza mimi ni mtendaji  maendeleo au  mtendaji maslahi” alisisitiza Malima.


Pamoja na hayo  mkuu wa mkoa aliasihi madiwani na  viongozi wengine  kuacha mara moja kuanzisha  migogoro isiyo na tija  , bali waelekeza nguvu zao  katika kusimamia miradi maendeleo ya wananchi na utoajiwa huduma bora.


Naye Mkuu wa Wilaya  Kilombero ,  Dunstan Kyobya alisema halmashauri hiyo alizindua mnada wa zao kokoa na bei ya Sh 25, 720 ambayo haujawahi  kutokea   na ulifanyika katika  ghala la Chama cha Msingi cha Wakulima (AMCOS) lililopo kata ya Mbingu, Mlimba.


Alisema fedha ambayo kwa mujibu wa Soko la Bidhaa Tanzania (TMX), inaingizwa moja kwa moja kwenye akaunti za wakulima na akaunti ya Halmashauri hiyo.


Kyobya alisema wanaendelea kuwahimiza   wananchi kuongeza bidii katika kilimo cha mazao ya kimkakati  kakao,  karafuu, michikichi , kahawa, pamba na ufuta.


Kwa upande wake  Mwenyekiti wa halmashauri  hiyo , Innocent Mwangasa alisema ,halmashauri yao imekuwa ni ya kuingwa ndani ya halmashauri zote za mkoa huo  ikiwemo ya ukusanyaji wa mapato imekuwa ikishika nafasi ya kwanza , usimamizi wa miradi  na sekta ya elimu.


Halmashauri hiyo imepata hati safi inayoridhisha kwa miaka mitano mfululizo na katika kikao hicho jumla ya hoja sita zilijadiliwa na zimepewa muda wa kukamilishwa ili ziweze kufutwa na CAG.


No comments: