THRDC ,Azaki watinga bungeni kutoa maoni muswada wa fedha,Wapongeza Wizara fedha kusikia kilio Cha Asasi za kiraia. - MAIPAC MEDIA TANZANIA

Breaking

MAIPAC MEDIA TANZANIA

A Centre for Indigenous and Pastoralists Community Informations




Sunday 23 June 2024

THRDC ,Azaki watinga bungeni kutoa maoni muswada wa fedha,Wapongeza Wizara fedha kusikia kilio Cha Asasi za kiraia.

 






Na:Mussa Juma,Maipac

maipacarusha20@gmail.com


Wadau kutoka sekta mbalimbali nchini,wakiongozwa  na mtandao wa watetezi wa Haki za Binaadamu (THRDC)leo wamekutana jijini Dodoma  kwa lengo la kutoa maoni yao na mapendekezo juu ya muswada  wa Fedha wa mwaka 2024 - (Financial Bill 2024).


Viongozi wa Asasi wakiongozwa na mratibu wa Taifa wa THRDC,Onesmo Ole Ngurumwa 

Licha ya kutoa maoni kadhaa kuboresha muswada huo pia wametoa pongezi kusikilizwa kilio cha AZAKi.


AZAKi pia zimeipongeza Wizara ya fedha kwa kukubali baadhi ya mapendekezo ya AZAKI ya muda mrefu kuhusu kurekebisha kifungu cha 64 cha Sheria ya Mapato ya Kodi kwa kupanua tafsiri ya Shirika la Hisani ( charitable organization) na kuongeza tasisi za afya na mazingira. 


Ole Ngurumwa alisema ,  ingawa maboresho haya ni madogo kulingana na mapendekezo ya AZAKi yaliyotaka kugusa maeneo yote yanayofanyiwa kazi na AZAKi kama msaada wa kisheria , Elimu ,  kupambana na ukatili wa watoto , utawala bora , haki za binadamu  lakini walau kuna maboresho.



Wengine waliowasikisha maoni ni pamoja na  Musa  Jonasi - Mwakilishi wa katibu Nacongo na Charlotte Kabunga -mwakilishi THRDC kanda ya kati .


"Tumekuja kushiriki katika  Mkutano huu   kwa ajili ya kutoa  uchambuzi uliofanywa juu ya mswada huu,  namna  unavyoweza kuathiri  uendeshaji wa shughuli mbalimbali za mashirika yasiyo ya kiserikali (NGOs)  hasa za kifedha na kikodi katika kutekeleza malengo za AZAKI "alisema ole Ngurumwa 


 Amesema lengo la  mapendekezo yao ni uboreshaji wa mswada huu  kwa manufaa Mashirika yasiyo ya kiserikali na ya taifa kiujumla.



"Tumewasilisha pendekezo kwa kamati namba ya kuboresha  tafsiri ya asasi ya hisani hapa nchini"alisema


THRDC kupitia wanachama wake Kila mwaka wamekuwa wakifanya uchambuzi wa bajeti,masuala ya Kodi na sheria mbalimbali ili kuboresha Utendaji wa AZAKi kwa manufaa ya umma.

No comments: