Moja ya mizinga ya nyuki inayopatikana kijijini hapo mtaalam akirina asali toka katika mzinga wa nyuki wataalam wakiwa katika kiwanda cha kuchakata asali kwa ajili ya kumfikia mlaji
NA: Mwandishi wetu, Maipac
Shirika la Chakula Duniani (FAO) linaeleza kuwa,Tanzania ni nchi ya pili kwa ufugaji nyuki barani Afrika baada ya Ethiopia.
Ubunifu
na ufugaji wa nyuki katika kijiji cha nyuki kilichopo mkoani Singida
kilichoanzishwa rasmi mwaka 2008 na kuzinduliwa na Waziri Mkuu Mstaafu,
Mizengo Pinda unathibitisha kuwa Tanzania tunaweza kuwa miongoni mwa
nchi vinara duniani kwa uzalishaji mazao ya nyuki na mazao yake na kuuza
katika masoko ya kimataifa.
Kijiji
hiki kipo takribani kilomita 12 kutoka Singida mjini kuelekea barabara
kuu ya Dodoma na kikiwa na jumla ya ekari 45,000 ambapo zipo katika Kata
za Kisaki, Ikungi, Iglansoni, Itigi Mkoani Singida na Kata ya Uyui
iliyopo mkoani Tabora.
Mwanzilishi
wa mradi huu ni Philemon Josephat Kiemi, almaarufu "Kiemi" ambaye ni
mhitimu wa shahada ya uzamili kutoka Chuo Kikuu cha Kilimo cha Sokoine
(SUA) akibobea katika masuala ya ufugaji nyuki kibiashara na kilimo .
Kiemi
anasema ameweza kutoa ajira za watu 114 ambao wana utalaam wa fani
mbalimbali kuhusiana na Kilimo, biashara na ufugaji wa nyuki kibiashara.
Anasema
licha ya kuwa na mradi wa nyuki katika eneo hilo pia amekuwa akipokea
watalii na watu mbali mbali kujifunza ufugaji nyuki na faida zake lakini
pia kushuhudia uhifadhi wa mazingira na kilimo rafiki na ufugaji
nyuki.
Kiemi
anasema alikuwa na ndoto ya kufanya jambo la kipekee katika ufugaji
nyuki na ndipo aliamua kwanza kujiendeleza na kupata elimu chuo kikuu
cha kilimo Sokoine na kabla ya hapo alisoma Hebrew University of
Jerusalem.
Mazao
ambayo yanapatikana katika kijiji hicho kwa sasa ni asali asilia
(Organic Honey)hii asali iliyopewa jina la "Singida Asali" au "IFONEO"
akiwa na upekee kutokana na utamu wake na harufi nzuri ambayo inatokana
na misitu asili ya singida.
Anasema
pia katika kijiji hicho wanazalisha bidhaa ya nyuki iliyopewa jina la
vumbi la singida ambayo inaimarisha kinga ya mwili, kuongeza vitamini na
protini mwilini lakini pia husaidia kukomesha tatizo la upungufu wa
nguvu za kiume.
Katika
kijiji hiki pia wanazalisha mishumaa inayotokana na nyuki; huu ni
Mshumaa ambao ni maalumu kwa kuwasha chumbani kwa ajili ya Kusafisha
hewa, kutoa Mwanga na kutoa harufu nzuri na pia sehemu ya matibabu ya
macho.
Kiemi
anasema pia wanazalisha sumu ya nyuki (Bee venom) ambayo inasaidia
kuongeza kinga ya mwili wa Binadamu kupambana na magonjwa ikiwepo Kansa
na kufubaza virusi vya UKIMWI huku ikiiacha seli hai zikiwa salama.
Anasema
wanazalisha Gundi ya nyuki hii ni bidhaa ya nyuki ambayo ni inazuia
Bacteria, fangazi na pia hutumika kama kipodozi na katika matumizi ya
kitabibu
Pia
katika kijiji hicho wanazalisha Maziwa wa nyuki (Royal jelly) hii ni
bidhaa ambayo humfanya mtu asizeeke mapema kwani huunganisha mwili na
kuupa uimara.
“Hii
ni bidhaa ya chakula pekee cha malkia wa nyuki kwenye Mzinga ambapo
malkia akila huishi miaka 3-5 na nyuki wengine wasiokula hichi chakula
huishi siku 55-60 toka kwenye yai”anasema
Anasema maziwa haya yanawavuta wanasayansi wengi kufanya utafiti uliopelekea binadamu wanaotumia zao hili kuchelewa kuzeeka.
Kiemi
anasema wanazalisha pia Supu ya nyuki (BEE BROOD) zao ambalo linatokana
na watoto wa nyuki lina protini nyingi. Wazee wengi na wavunaji wa
asali wanatafuna masega yakiwa na matoto yale pamoja.
“Hii kwa historia inasadikika wanaokula hivi wawaumwi maradhi mbalimbali mara kwa mara”anasema
Mkurugenzi
huyo anasema katika kijiji hicho, pia wanatoa elimu ya ufugaji nyuki na
huduma nyingine zitokanazo na nyuki ikiwepo utengenezaji wa Mizinga,
Mitego ya chavua ya nyuki na mavazi ya kujikinga na nyuki .
“pia
tunatoa Mafunzo ya Ufugaji wa nyuki Kibiashara kwa Vitendo na watu
wengi wanafika hapa kujifunza na kwa anataka maelezo zaidi awasiliane
nasi ”anasema
Aelezea maajabu ya kijiji hicho.
Akielezea
kijiji hicho, ndugu Suphian Juma ambaye ni Mwanasiasa na Mdau wa
masuala ya Utalii, alipoenda kupata mapumziko kijijini hapo ,anasema
ameshangazwa na ubunifu mkubwa katika kijiji hicho ambao licha ya
kuzalisha mazao ya nyuki pia kuna pori kubwa la miti ya asili yenye
urefu wa wastani kuna nyumba kadhaa za rangi ya karoti zikijengwa
mbalimbali huku umeme na miundo mbinu ya maji ikisambazwa huko ndani
kikamilifu.
Juma
anasema katika kijiji hicho kila nyumba ina matumizi yake, zipo nyumba
za Makazi, ofisi, viwanda na kadhalika jambo ambalo limefanywa na
ubunifu mkubwa.
“Hii
ni Uwekezaji unastahili kuitwa na kubeba maantiki ya neno "kijiji" kwa
kuzingatia tafsiri ya kuona mwingiliano wa shughuli za ufugaji wa nyuki,
Makazi ya Watu (wafanyakazi), miundo mbinu ya huduma za kijamii, miti
asilia, ndege, wanyama kama digidigi, Sungura na kadhalika”anasema.
“Baada
ya kuelezwa mengi juu ya mradi huu nilipelekwa kiwanda cha kutengeneza
mizinga ambapo nilijionea vijana wengi wa kike na wa kiume wakitengeneza
mizinga mizuri sana, kuanzia kwenye muonekano hadi kwenye uimara
“anasema
Anasema
kijiji hicho kimeweza kuwa na uwezo wa kufunga mashine za kisasa
kutengeneza asali na mazao mengine jambo ambalo ni kivutio kikubwa.
“kijiji
hicho ni mfano tosha kwa kile ambacho amekuwa akihimiza Rais Samia
suluhu vijana kujitokeza kujiajiri na serikali itaendelea kuwapa
mazingira mazuri ya kufikia malengo yao”anasema Suphian
Juma
anatoa wito kwa watanzania kutoka maeneo mbalimbali na watalii kufika
katika kituo kijiji hicho, kuona mazao ya nyuki lakini pia kujifunza
ufugaji nyuki wa kisasa na kibiashara.
Rehema Nkuwi anasema katika kijiji hicho, kuna mengi ya kujifunza ikiwepo utunzwaji mzuri wa mazingira.
“hapa
tunajifunza uvunaji wa asali bila kuathiri maisha ya nyuki lakini pia
jinsi ya kuchuja asali na kuihifadhi ili isiharibike”anasema
Nkuwi
anasema huduma ambazo zinatolewa ,katika kijiji hicho, ikiwepo maeneo
ya kulala wageni, vyakula na mahitaji mengine inaonesha vijana wa
kitanzania wakipewa fursa wanaweza kufanya maajabu.
Hiki
ndicho kijiji cha nyuki ambacho kina maajabu ya aina yake ikiwepo
ubunifu katika uandaaji mazao ya nyuki, uvunaji wa nyuki na uandaaji ya
mashamba ya nyuki na kuwa eneo la kivutio cha utalii.
No comments:
Post a Comment