MAAFISA ELIMU WILAYA YA KIBAHA WAJENGEWA UWEZO MASUALA YA VVU/UKIMWI - MAIPAC MEDIA TANZANIA

Breaking

MAIPAC MEDIA TANZANIA

A Centre for Indigenous and Pastoralists Community Informations




Wednesday 1 March 2023

MAAFISA ELIMU WILAYA YA KIBAHA WAJENGEWA UWEZO MASUALA YA VVU/UKIMWI

 

 

Mratibu wa UKIMWI wa Halmashauri ya Mji Kibaha Siwema Cheru akifundisha maafisa elimu kata  katika semina ya VVU na Ukimwi mjini Kibaha

 
NA: JULIETH MKRERI, MAIPAC KIBAHA


HALMASHAURI ya Mji Kibaha imeendesha semina ya kuwajengea uwezo maafisa Elimu kata,walimu wa shule za Msingi na Sekondari kuhusiana na masuala ya VVU/UKIMWI mahala pa kazi kwa lengo la kuondoa unyanyapaa na ukatili wa kijinsia.

Mratibu wa UKIMWI wa Halmashauri ya Mji Kibaha Siwema Cheru amesema semina hiyo ni mwendelezo wa Mafunzo mengine ambayo yamekuwa yakitolewa kwa wadau mbalimbali ili kuondoa vitendo vya unyanyasaji sehemu za kazi na kwamba sasa wamefikiwa waratibu wa Elimu kata na walimu ambao ni wadau wakubwa kwenye jamii na wanakaa na wanafunzi muda mrefu.
Baadhi ya Walimu wakiwa katika semina ya VVU na Ukimwi


Mwezeshaji katika  semina hiyo Dk.Mariam Ngaja ameeleza kuwa kupitia semina hiyo witawajenge uelewa walimuwa na watakuwa na wanawajibu wa kuwafundisha wanafunzi wao kuhusu  afya ya uzazi kwa Vijana na maradhi yanayoambukizwa kwa njia ya ngono na Elimu ya dawa ya kulevya.

Ngaja ameongeza kuwa semina hiyo ambayo ni ni ya kawaida na ni utekelezaji wa mkakati wa nne wa Taifa wa kudhibiti UKIMWI Tanzania hasa kwa wasichana balehe, Vijana na wanawake.

 Mmoja wa walimu Augustine Seso ameishukuru Halmashauri kwa kuwapatia  semina hiyo na kwamba imewafikia muda muafaka na sasa wanakwenda kwenye jamii kutimiza lengo la kutoe Elimu ili kuondosha unyanyasaji na ukatili wa kijinsia kwenye jamii.
Picha ya pamoja mara baada ya kupata mafunzo kwa maafisa elimu hao

No comments: