GODBLESS LEMA akisalimiana na wakazi na wanachama wa Chadema waliojitokeza kumlaki |
Baadhi ya wakina Mama wakiiimba nyimbo za kumsifia Lema |
Baadhi ya VIJANA WA chadema wakiwa tayari kwa msafara wa kurudi Arusha na Mjumbe wa kamatinkuu ya chadema |
Msafara wa GODBLESS LEMA ukiwa njiani kuelekea ARUSHA |
Baadhi ya VIJANA WA chama hicho wakiiimba nyimbo za kumpongeza Lema |
Askari POLISI wakihakikisha usalama unakuwepo Muda wote |
Na; Mwandishi wetu, KIA
Aliyewahi kuwa Mbunge wa Arusha mjini kupitia Chadema, Godbless Lema hatimaye amerejea nchini, akitokea uhamishoni nchini Canada na amepokewa katika uwanja wa ndege wa kimataifa ya Kilimanjaro na viongozi kadhaa wa Chadema na Viongozi wa dini.
Lema baada ya kushuka katika ndege ya shirika la Ethiopian alielekezwa moja kwa moja chumba Cha wageni maarufu(VIP) na kupokelewa na viongozi mbalimbali wa chama hicho.
Baadae Lema alifanya mazungumzo kidogo na viongozi wa chadema na Sasa msafara umeanza kuelekea Arusha.
Lema aliwasalimia viongozi wote waliofika kumpokea na amewapungia mkono mamia ya wanachadema waliokuwa nje ya VIP vikiwepo vikundi kadhaa vya Ngoma.
Ikumbukwe Lema aliondoka nchini mara baada ya uchaguzi Mkuu mwaka 2020 Ili kuokoa maisha yake kwa kile ambacho ameeleza kupokea vitisho vya kisiasa.
No comments:
Post a Comment