RC KUNENGE AFANYA ZIARA SINO TAN KUSHUHUDIA MAENDELEO YA UJENZI WA VIWANDA 300 - MAIPAC MEDIA TANZANIA

Breaking

MAIPAC MEDIA TANZANIA

A Centre for Indigenous and Pastoralists Community Informations




Monday 6 March 2023

RC KUNENGE AFANYA ZIARA SINO TAN KUSHUHUDIA MAENDELEO YA UJENZI WA VIWANDA 300



MKUU wa Mkoa wa Pwani Abubakar Kunenge akipewa maelezo na wataalam kiwandani hapo


MKUU wa Mkoa wa Pwani Abubakar Kunenge akioneshwa utekelezaji katika kiwanda cha Sino Tan


MKUU wa Mkoa wa Pwani Abubakar Kunenge alipotembelea kiwanda cha Sino Tan

 

 JULIETH MKIRERI , MAIPAC KIBAHA

maipacarusha20@gmail.com 

MKUU wa Mkoa wa Pwani Abubakar Kunenge ametembelea katika kongani ya viwanda ya Sino Tan iliyopo Kwala wilaya ya Kibaha kukagua maendeleo ya ujenzi.

Akizungumza na Waandishi wa Habari Kunenge amesema amefanya ziara hiyo kuona maendeleo ya mradi huo ambao ni wa uwekezaji mkubwa wa viwanda zaidi ya 300 katika mkoa huo.

Amesema kiwanda cha kwanza katika Kongani hiyo kitaanza kufanya kazi Juni na ajira 5000 zitatolewa na mradi ukikamilika  ajira 100,000  kwa awamu ya kwanza zitapatikana.

"Ahadi yangu eneo hili litakuwa kubwa kwenye uwekezaji na wanaoanzisha Kongani watakuja kujifunza hapa mpangiliio na kila kitu" amesema.

Aidha Mkuu huyo wa Mkoa amesema baada ya kikao hicho na kufanya mkutano wa pamoja na wataalamu kutoka kwenye Taasisi watakuwa na utaratibu wa kukutana mara kwa mara kutatua vikwazo vinavyojiyokeza kwenye mradi huo ili uweze kukamilika kwa wakati.

" Tumekubaliana hizi taasisi zinazohusika na kuunganisha huduma kwenye hii kongani zikutane na uongozi wa SINO TAN ili waonyeshwe ramani hii itasaidia kutoharibu miundombinu na kupunguza gharama za ziada" amesema Kunenge.

Kwa mujibu wa Kunenge Wakala wa Maji na Usafi wa Mazingira Vijijini (RUWASA) wanatarajia kutatua kikwazo cha maji mwezi huu huku mahitaji ya umeme wa Megawat 50 yakiwa yanashugjulikiwa na Tanesco na kufikia Juni tatizo katika huduma hizo litakuwa limeisha.

Mwenyekiti wa Kongani hiyo Janson Huang amesema ifikapo June mwaka huu kituo cha huduma kitakuwa kimekamilika na kiwanda cha kwanza kitaanza kazi.

Katika ziara hiyo Kunenge ameambatana na Watendaji kutoka katika ofisi yake na Taasisi wezeshi zitakazohusika kufikisha huduma katika eneo hilo wakiwemo TANESCO, TARURA, RUWASA na DAWASA .

No comments: