WANAWAKE ARUSHA WAUNGANA KUKEMEA UKATILI NA UNYANYASAJI WA KIJINSIA - MAIPAC MEDIA TANZANIA

Breaking

MAIPAC MEDIA TANZANIA

A Centre for Indigenous and Pastoralists Community Informations




Friday 3 March 2023

WANAWAKE ARUSHA WAUNGANA KUKEMEA UKATILI NA UNYANYASAJI WA KIJINSIA



Baadhi ya wakina Mama WA KKKT Jimbo la Arusha wakiwa katika semina



Na Onesmo Elia Mbise -Arusha


Katika Kuelekea Kilele Cha  Maadhimisho Ya Siku Ya wanawake Duniani, Idara ya wanawake katika Kanisa La kilutheri Tanzania Jimbo La Arusha mashariki Dayosisi Ya Kaskazini Kati  Wamekemea Ukatili Kwa Wanawake Pamoja Na Unyanyasaji w Kijinsia Unaendelea katika Mkoa wa Arusha  na Maeneo Mengine ya Nchi ya Tanzania.


Mwenyekiti wa Wanawake Jimbo La Arusha Mashariki Nembris Samweli ameeleza kuwa Dunia Ya Sasa Imejaa Ukatili wa Kijinsia Haswa Kwa Wanawake na watoto wadogo na katika Hili wanawake Wote Duniani wanapaswa kuungana na kuelimisha Jamii Ili Kuondokana Na Ukatili  na Unyanyasaji wa  Kijinsia.


"Tunapoelekea Katika Kilele Cha Maadhimisho ya wanawake Duniani sisi wanawake Tunapaswa kuungana pamoja na kupinga Ukatili Wa kijinsia Kwa watoto wa kike kwani Kina Mama Ndio walezi wa Familia Zetu"


Nembris Amesema kuwa Wanawake ndio walezi wa Familia kuanzia ngazi ya kulea  watoto Kiakili, na  kueleza Jamii jinsi ambapo Familia nyingi zinapitia matatizo Kwa Kuwaona  Ndgu zao wakifanyiwa Ukatili, na Hata Ubakaji.


Naye  Narivi Peta Kyamba Amesema kuwa Mwanamke akisimama katika Jamii atalisimamisha Taifa kiuchumi, kijamii na Hata katika Nyanja za Kiungozi hvyo Wanawake wanaweza kuleta Mabadiliko  katika Kutokomeza Ukatili na Unyanyasaji kwenye Jamii.


Amesema Kuwa Mwanaumke Anaweza kusimamisha Uchumi wa Nchi kwani wanawake ndio nguzo katika Familia na kwamba katika Dunia Ya Sasa wameongeza Nguvu katika Kujimarisha kiuchumi.


Ukatili na Unyanyasaji wa Kijinsia  tayari inaonekana Kuwa ni Changamoto Kwa Jamii za mikoa Ya Kaskazini na Tanzania  Kwa Ujumla.

No comments: