MJI WA KIBAHA WAWAJENGEA UWEZO WAKUNGA KUTOA HUDUMA ZAHANATI YA MWENDAPOLE - MAIPAC MEDIA TANZANIA

Breaking

MAIPAC MEDIA TANZANIA

A Centre for Indigenous and Pastoralists Community Informations




Thursday 20 April 2023

MJI WA KIBAHA WAWAJENGEA UWEZO WAKUNGA KUTOA HUDUMA ZAHANATI YA MWENDAPOLE

 


 

NA JULIETH MKIRERI, MAIPAC KIBAHA


maipacarusha20@gmail.com 

HALMASHAURI ya Mji Kibaha kupitia Zahanati ya Mwendapole iliyopo Kata ya Kibaha imeratibu jopo la Wakunga wabobezi wanaotarajia kutoa Elimu kwa wajawazito Aprili 6, 2023 ili kunusuru afya ya Mama na Mtoto wakati na baada ya kujifungua.

Hayo yameelezwa mjini Kibaha  na Prisca Nyambo  msimamizi wa huduma za uzazi Kibaha ambaye pia ni Mkunga ambaye alitaja huduma zitakazotolewa kuwa ni uchunguzi wa kina na maendeleo ya ujauzito Maandalizi ya Kujifungua, Uchunguzi wa  dalili za hatari kwa mjamzito, lishe bora,upimaji wa vipimo mbalimbali pamoja na kutoa ushauri.

Nyambo amesema Zahanati ya Mwendapole imekuwa na wateja wengi wa kujifungua kutokana na huduma bora zinazotolewa kwani takwimu zinaonyesha kuwa kati ya wajawazito 140 hadi 180 hupokewa kwa Mwezi kuanza huduma za Kliniki.

Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji Kibaha Mshamu Munde amesema nia ya Serikali ni kupunguza ama Kuondoka kabisa vifo kwa wajawazito na watoto ambapo alitoa rai kwa Wakunga wote kuwa karibu na wajawazito na wawe na kanzi data maalum itakayowasaidia kuwafuatilia.

Naye  Diwani wa Kibaha Goodluck Manyama ameishukuru Serikali  kupitia Halmashauri ya Mji Kibaha kwa kufanya utaratibu huo ambao unakwenda kutoa uhakika wa afya za Watoto watakaozaliwa 

Halmashauri ya Mji Kibaha yenye hospitali,Vituo vya afya na Zahanati 25 zinazotoa huduma ya Mama na Mtoto,kwa Mwezi hupokea kati ya akina mama 600 hadi 650 wanaofika kujifungua.

Inmeelezwa kuwa utaratibu kama huo ni kwa mara ya kwanza kufanyika katika zahanati hiyo na unatarajiwa kufika katika maeneo mengine ya Kongowe,Msangani na Viziwaziwa.

No comments: