RC KUNENGE AZINDUA DARAJA MKURANGA - MAIPAC MEDIA TANZANIA

Breaking

MAIPAC MEDIA TANZANIA

A Centre for Indigenous and Pastoralists Community Informations




Wednesday 26 April 2023

RC KUNENGE AZINDUA DARAJA MKURANGA

 

 


Mkuu wa Mkoa wa Pwani Abubakari Kunenge akizungumza wakati WA uzinduzi wa daraja





NA JULIETH MKIRERI, MAIPAC MKURANGA



MKUU wa Mkoa wa Pwani Abubakar Kunenge Aprili 26, 2023 amezindua Daraja la Mipeko iliyopo Barabara ya Mwanambaya lililojengwa kwa gharama ya sh Milion 214.

Akizungumza na  Wananchi wa Mipeko  Kunenge amepongeza Rais  Dkt Samia Suluhu Hassan  kwa kuleta Maendeleo ambayo yanawagusa wanachi wa kawaida.

Mkuu huyo wa Mkoa amebainisha kuwa Rais Samia  alipofanya ziara Mkoani Pwani alieleza nia yake ya kuhakisha Mkoa huo unapata miundombinu yote Muhimu ya Afya, Elimu, Maji, Nishati, Barabara.

Ameshikuru kwa namna ambavyo utekelezaji unaendelea na kwamba Mkoa huo una Mtandao wa Barabara wa km 6629 zinazohudumiwa na TANROADS na TARURA. 

Amesema Bajeti ya kutekeleza  shughuli za Barabara kwa mwaka 2021/22 ilikuwa ni Bilion75.5 na kwa mwaka 2022/23 imeongezwa kufikia Bilion 81.

Ametoa maelekezo kwa Mkurugenzi wa  Halmshauri ya Mkuranga kupanga Mji wa Mkuranga kwa kuwa Mji huo unakuwa kwa kasi na kwamba Serikali inafanyia kazi maombi ya Wananchi hao ya kujengewa Kituo cha Afya, kupelekewa Umeme na ujenzi wa Daraja.


No comments: