WATU WANNE WA FAMILIA MOJA WAFARIKI DUNIA BAADA YA GARI KUSOMBWA NA MAJI WILAYANI ARUMERU - MAIPAC MEDIA TANZANIA

Breaking

MAIPAC MEDIA TANZANIA

A Centre for Indigenous and Pastoralists Community Informations




Tuesday 25 April 2023

WATU WANNE WA FAMILIA MOJA WAFARIKI DUNIA BAADA YA GARI KUSOMBWA NA MAJI WILAYANI ARUMERU

 

Baadhi ya wananchi na askari wakiotoa miili ya waliopoteza maisha katika ajali hiyo

Na Mwandishi wetu 


maipacarusha20@gmail.com

Watu wanne wa familia moja wamefariki dunia na wengine wawili wameokolewa baada ya gari waliokuwa wamepanda kusombwa na mafuriko ya maji katika eneo la Kin’gori kata ya Malula Wilaya ya Arumeru mkoani Arusha mapema leo


Akizunguma na wanahabari KATIKA eneo la tukio mkuu wa wilaya ya Arumeru Mh Emanuela Kaganda amesema kuwa  gari iliyosombwa na maji ni aina ya Noah yenye Namba za usajili T 499 DMY.

 Amesema gari hilo lilikuwa na abiria Sita ambao ni Naiman Metili, Anjela Metili (36),Colin Mathayo Lyimo (16) ,Lisa Metili (8) ,Brenda Amani (25) ,Martha Metili (40).


Mkuu wa Wilaya amesema kuwa waliofanikiwa kuokolewa ni Naiman Metil ambaye alikuwa Dereva wa gari hiyo Pamoja na Anjela Metili ambaye kwasasa anapatiwa matibabu katika hospital ya  Boma wilayani Hai.

Lakini wengine wote wamefariki ambapo mpaka sasa miili iliyopatikana ni watu watatu huku mtoto Lisa akiendelea kutafutwa kwasababu maji yaliyomsomba yalimpeleka mbali Zaidi 


Mheshimiwa Kaganda ametoa wito kwa madereva na watembea kwa miguu kutokuingia katika maji yanayovuka barabara ili kujiepusha na madhara ya mvua kubwa inayonyesha kwa Sasa.

No comments: