WANACHAMA KAGERA UMOJA ASSOCIATION WATAKIWA KUENDELEA KUSHIRIKIANA PAMOJA - MAIPAC MEDIA TANZANIA

Breaking

MAIPAC MEDIA TANZANIA

A Centre for Indigenous and Pastoralists Community Informations




Saturday 13 January 2024

WANACHAMA KAGERA UMOJA ASSOCIATION WATAKIWA KUENDELEA KUSHIRIKIANA PAMOJA

 

Wanachama wa KAGERA UMOJA ASSOCIATION (KUA) Wakicheza nyimbo za asili ya Mkoa wa KAGERA.

Wanachama wakiburudika Kwa nyimbo za asili

Mwenyekiti wa KAGERA UMOJA ASSOCIATION Gosbert Shausi  akizungumza na wanachama katika sherehe za kuaga mwaka 2023 na kuukaribisha mwaka 2024


Na Lilian Kasenene, Morogoro 


maipacarusha20@gmail.com


Kikundi Cha Kagera Umoja Association(KUA) kilichopo mkoani Morogoro katika sherehe kuaga Mwaka 2023 na kukaribisha Mwaka mpya wa 2024, kimewataka wanaumoja huo kuendelea kushirikiana, pamoja na kukumbukana kwenye Raha na shida.


Akizungumza wakati sherehe hiyo mwenyekiti wa Gosbert Shausi alisema wanaumoja huo wamekuwa wakifanya sherehe hizo kila Mwaka na wamekuwa wakijumuika na familia zao.


Shausi alisema pamoja na kukutana kwao kila Mwezi na kuzumgumza mambo wamefanikiwa kuwa na uwanja ambapo wameanza ujenzi na ndipo patakuwa sehemu ya kukutania wanaumoja hao.


Alisema sherehe yao ya mwaka huu  imekuwa na utofauti ambapo wameacha kufanyia kwenye kumbi za ndani na Sasa kutoka nje ya mji ikiwa ni pamoja na kuangalia vivutio  vilivyopo kwenye milima ya uluguru.


"Tumefanya huku nje ya mji ili wanachama waone vivutio na kuangalia mandhari nyingine na sasa tumekuja huku," alisema Mwenyekiti huyo.


Mmoja wa wanaumoja huo wa KUA Loveness Nyawili alisema kukutana kwao kunawajenga kuendeleza upendo pamoja na kushikamana zaidi katika Kila hari.


Katika sherehe hiyo nyimbo mbalimbali za kabila la wahaya kutoka mkoani Kagera zilipigwa na wanaumoja kuzicheza kwa furaha.


No comments: