Watakiwa kutumia Kilimo Ikolojia kuongeza uzalishaji mazao na kulinda afya za walaji - MAIPAC MEDIA TANZANIA

Breaking

MAIPAC MEDIA TANZANIA

A Centre for Indigenous and Pastoralists Community Informations




Tuesday 5 March 2024

Watakiwa kutumia Kilimo Ikolojia kuongeza uzalishaji mazao na kulinda afya za walaji



Wadau wa Kilimo na ufugaji IKOLOJIA wakizungumza na MAIPAC Media Tanzania 



Mratibu warsha hiyo, Erimelinda Temba akizungumza na wadau wa kilimo


Na: Mussa Juma, maipac


maipacarusha20@gmail.com


Wakulima na wafugaji nchini, wameshauriwa kutumia mbinu za asili katika Kilimo na Ufugaji (Kilimo Ikolojia) ili kupunguza matumizi makubwa ya dawa za viwandani.


Kilimo na Ufugaji wa asili pia mazao yake yana bei za juu katika Soko la Dunia na ni Salama zaidi kwa afya za walaji na wakulima.


Mkurugenzi wa Taasisi ya ECHO EAfrika Erwin Kinsey  alitoa ushauri huo,katika warsha  ya wadau wa Kilimo Ikolojia mkoa Arusha ambayo iliwashirikisha wakulima, wafugaji na wanafunzi wa vyuo vya Kilimo na Watendaji wa Serikali ambayo ilifanyika jijini Arusha.


Kinsey alisema, wakulima na wafugaji wanaujuzi wa asili ambao ni bora zaidi kuliko Kilimo cha kisasa ambacho kina matumizi makubwa ya kemikali kuanzia kulima, kupanda, kuvuna na kuhifadhi mazao.


"Tuendeleze Kilimo Ikolojia kwani pia ni Salama zaidi kwa Afya ya mkulima na mlaji mfano wagogo wana mbinu nzuri za kutunza mazao Yao bila dawa tujifunze "alisema


Mratibu warsha hiyo, Erimelinda Temba alisema warsha hiyo hufanyika Kila mwaka ili kuendelea uzalishaji wa Kilimo lkolojia ili kuwa na uzalishaji endelevu wa chakula.


Temba alisema kuna umuhimu wa kuwa na Ufugaji na Kilimo Ikolojia ili  kuboresha uchumi wa Jamii kwa ujumla kwa gharama nafuu zaidi.


"Unatumia mbolea ya mifugo katika Kilimo, unatumia dawa za asili Katibu Mifugo lakini pia unatumia wadudu waliopo ardhini kuboresha Afya ya ardhi na wengine kusaidia kutibu magonjwa "alisema


Mwenyekiti wa vikundi vya Maendeleo vya wakulima na wafugaji Longido, Nambori Nabaki alisema Kilimo Ikolojia kimekuwa na manufaa kwao kwani wanapunguza gharama za mbolea za viwandani na dawa za Mifugo.


Hata hivyo aliomba wafugaji kusaidiwa kupata tiba ya ugonjwa wa mbuzi na Kondoo wa Olmiro ambao umeanza kuuza Mifugo Yao 


Akizungumzia ugonjwa huo Daktari wa Mifugo wa Halmashauri ya Arusha DC, Linus Prosper alisema ugonjwa huo unasambazwa na mbwa na kuwataka wafugaji kuchanja mbwa wao.


"Ugonjwa huu unatokana na minyoo ya mbwa na husambazwa kupitia kinyesi chake na mbuzi na Kondoo wakila nyasi zenye kinyesi wadudu  huingia hadi kichwani na kumfanya mbuzi au Kondoo awe na kizunguzungu na asipopata tiba ambayo hufa"alisema 



Mwenyekiti wa vikundi vya Maendeleo vya wakulima na wafugaji Longido, Nambori Nabaki akizungumza na waandishi wa Habari nje ya warsha hiyo

No comments: