WASHINGTON DC
maipacarusha20@gmail.com
Waziri wa Viwanda na Biashara, Mhe. Dkt. Selemani Jafo akiwa ameambatana na Katibu Mkuu wa Wizara hiyo Dkt Hashil Abdallah wakishiriki Mkutano wa Majadiliano wa Mawaziri wa Biashara wa nchi za Afrika zinazonufaika na Mpango wa AGOA, uliofanyika Julai 24, 2024, Makao Makuu ya Benki ya Dunia, Washington, Marekani.
Mkutano huo ni maandalizi ya Msimamo wa Afrika katika kusisitiza kuongezewa muda kwa kipindi cha miaka isiyopungua 16 ili uweze kutabirika na kuruhusu miradi mikubwa ya uwekezaji wa muda mrefu. Msimamo huo utawasilishwa kwenye Kongamano la 21 la Mpango wa AGOA linaloendelea kufanyika kuanzia tarehe 24-26 Julai 2024, Washington, Marekani.
No comments:
Post a Comment