Na: Mwandishi Wetu maipac
maipacarusha20@gmail.com
Shirika la waandishi wa Habari jamii za pembezoni MAIPAC kesho wanatatajia kuzindua mradi wa Uhifadhi wa mazingira kwa kutumia maarifa ya asili awamu ya pili.
Akizungumza na waandishi wa habari mjini Karatu Mkurugenzi mtendaji wa Maipac Mussa Juma amesema kuwa mradi huo utazinduliwa na Mwenyekiti wa Halmashauri ya Monduli Isack Joseph katika ukumbi wa Makambo -Te Makuti uliopo eneo la Kigongoni mto wa Mbu
Amesema mradi huu ni sehemu ya pili ya mradi wa Uhifadhi mazingira kwa maarifa ya asili uliohusisha jamii za Maasai ila Sasa utaangazia jamii za wahadzabe na wadatoga.
No comments:
Post a Comment