UWANJA NANE NANE KANDA YA MASHARIKI KUBORESHWA ILI KUWA HADHI YA KIMATAIFA . - MAIPAC MEDIA TANZANIA

Breaking

MAIPAC MEDIA TANZANIA

A Centre for Indigenous and Pastoralists Community Informations




Sunday 21 July 2024

UWANJA NANE NANE KANDA YA MASHARIKI KUBORESHWA ILI KUWA HADHI YA KIMATAIFA .

 






Na Lilian Kasenene,Morogoro


maipacarusha20@gmail.com


MKUU wa mkoa wa Dar es Salaam, Albert Chalamila amesema mpango mkakati umeandaliwa na kuwasilishwa Wizara ya Kilimo  na kupitia wadau kuweza kupata fedha za kuuboresha zaidi viwanja vya maonesho wa Nane Nane wa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere , Kanda ya Mashariki ili uwe na hadhi ya kifaifa na kimataifa.


Chalamila alisema hayo mjini Morogoro wakati wa kikao cha maandalizi ya Nane Nane ya Kanda ya Mashariki yanayofanyika Viwanja vya Mwalimu Julius Kambarage Nyerere na  kujumuisha halmashauri za mikoa ya  Tanga, Pwani , Dar es Salaam na Morogoro.


“Mtakumbuka kwa miaka mingi tumekuwa na uwanja ambao bado haina hadhi kubwa , lakini sasa kuna andiko ambalo linaandaliwa na ambalo litapelekwa wizara ya Kilimo , tunaamini pia kupitia wadau , uwanja wetu unaweza kupata fedha za kuuboresha zaidi “alisema Chalamila.


Mkuu huyo wa mkoa alitaja baadhi ya maeneo ya maboresho  ni kwenye  mwonekano wa majengo,  miundombinu ya barabara  na maji , kuwa na maeneo ya  mapumzuko , maeneo ya  kuvutia michezo mbalimbali ya watoto na watu wengineo .


Pia alisema kilimo  kinapaswa kuwa na mlengo mkubwa wa kuwasaidia wakulima na wafugaji, hivyo ni wajibu  kuyaboresha maonesho ya Nane Nane  kwa kuhamasisha zaidi, kuwa na wadau mbalimbali ambao wanaweza kuhudhuria kuonesha  na wanaoweza kuhudhuria kununua  bidhaa zao.


Chalamila alisema ni muhimu zaidi kuona namna ya kumkutanisha wakulima , wafugaji na masoko pale  wanapoleta bidha zao  badala ya kuamini ya kwamba  wanakuja kuionesha.


“ Sisi tunafurahia kuziona kwani kikubwa wanaleta bidhaa zao ili kuiona , kuzipenda na kuweza kuzinunua” alisema Chalamila.


Mkuu wa mkoa huyo  alitumia fursa hiyo kuwahamasisha wananchi wote kuwa waamshwe na kengere  ya Nane Nane , kwani Nane Nane yam waka huu (2024) ni ya kipekee kutokana na kuwepo kwa mvua nyingi lakini hazijaathiri upatikanaji wa mazao.


 “ Ni baadhi ya maeneo machache yameathirika kidogo hasa kwenye mazao ya mpunga ambacho kinatengemea kiwango fulani cha maji mashambani lakini kwa asilimia kubwa mazao yamepatikana  “aliisema


Mkuu wa mkoa aliwataka wananchi kujitokeza kwa wingi kwenye viwanja hivyo kuona vipando , kuona mazao , mifugo na kuona teknolojia mbalimbali za kilimo, mifugo na uvuvi  hasa ikizingatiwa katika zama hizi  ni kilimo  kinacholenga zaidi udhibiti kasi ya mabadiliko ya tabianchi.


Kwa upande wake  Katibu Tawala wa mkoa wa Morogoro, Dk Mussa Ali Mussa alisema  Sh milioni 50 zimetolewa kwenda  mamkala ya  usimamizi wa huduma ya   maji ili kuchimba visima viwili kwa ajili ya  matumizi ya umwagiliaji vipando na  mengine .



No comments: