VIJANA KONDOA KUNUFAIKA NA MKOPO WA BODABODA - MAIPAC MEDIA TANZANIA

Breaking

MAIPAC MEDIA TANZANIA

A Centre for Indigenous and Pastoralists Community Informations




Tuesday, 31 January 2023

VIJANA KONDOA KUNUFAIKA NA MKOPO WA BODABODA

 

Mjumbe wa Halmashauri Kuu Taifa Muhsin Ussi akisalimiana na Wazee wa chama Cha Mapinduzi Wilayan Kondoa baada ya kuzindua tawi la vijana wa chama Cha Mapinduzi (UVCCM) wanapjishulisha na kazi ya Bodaboda

Shakila Nyerere, MAIPAC Doodma


Mjumbe wa Halmashauri Kuu CCM Taifa, Muhsin Ussi amewahakikishia vijana wa Tawi la UVCCM CITY CENTRE kupatiwa mikopo ya  pikipiki li wajiajiri na wajikwamue kiuchumi.

 Tawi hilo limezinduliwa Leo Wilayani Kondoa Mkoani Dodoma ambapo ufunguzi huo umefanyika sambamba na Sherehe za Kuadhimisha Miaka 46 ya kuzaliwa kwa Chama cha Mapinduzi (CCM) Tanzania tangu kilipozaliwa Mwaka 1977.

Akizungumza na Vijana hao Muhsin Ussi Amesema Serikali  ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania, inataka mapato ya Ndani ya Halmashauri yatenge Asilimia (10%) kwa ajili ya mikopo kwa vikundi, ambazo zimegawanywa katika Makundi Matatu,Asilimia (4%) kwaajili ya kundi la akina Mama,Asilimia (2%) Kundi la Vijana wenye uhitaji Maalumu na Asilimia (4%) Nyingine inawagusa Vijana moja kwa moja.

Kutokana na Asilimia (4%) ya Fedha iliyotengwa kwaajili ya Vijana, Ndg.Muhsin ametoa Ahadi ya kuwahakikishia vijana wa Tawi hilo kuwa Halmashauri inawapatia Fedha kwaajili ya kununua Bodaboda.

"Fedha hizi zimewekwa na Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan kutatua Changamoto za Vijana Lazima Vijana wazipate Fedha hizi, Ikiwa kuna mtu yeyote alikuwa anatumia Janjajanja kukwepesha Fedha hizi zisiwafikie Vijana waliokusudiwa, Huyo mtu tunampa Salamu arobaini yake imefika".Amesema Ussi.

No comments: