WAANDISHI WA HABARI WATAKIWA KUIELEZA JAMII PROGRAM YA SHULE BORA. - MAIPAC MEDIA TANZANIA

Breaking

MAIPAC MEDIA TANZANIA

A Centre for Indigenous and Pastoralists Community Informations




Friday, 27 January 2023

WAANDISHI WA HABARI WATAKIWA KUIELEZA JAMII PROGRAM YA SHULE BORA.

Katibu Tawala Mkoa wa DODOMA Dk. Fatuma Mganga akizungumza na wanahabari hawapo pichani 



SHAKILA NYERERE, MAIPAC DODOMA

KATIBU tawala Mkoa wa Dodoma Dk.Fatuma Mganga amefungua mafunzo ya program Shule Bora kwa waandishi wa Habari Mkoa wa Dodoma wilayani Kondoa.

Amesema kuwa swala la Elimu katika Mkoa wa Dodoma bado halijatangazwa vizuri na kuwataka waandishi wa habari wakawe chachu cha kuielimisha jamii.

Amempongeza Rais Samia Sulluhu Hassan Kwa jitihada zake za dhati za kuongeza pesa za maendeleo katika mkoa wa Dodoma ambapo shilingi bilioni 7.8 zimetolewa na kuwezesha kujenga vyumba vya madarasa 393 ya shule za msingi na madarasa 130 yamejengwa Kwa shule za sekondari kwa gharama ya  shilingi bilioni 20

Aidha amewaeleza waandishi wa habari kuwa Rais Samia ameongeza bajeti ya Elimu bila malipo Kwa shule za misingi na sekondari.

Pamoja na jitihada hizo za serikali amewataka wazazi kushirikiana na serikali katika ujenzi na uhifadhi wa Miundombinu ya elimu ikiwemo ya madarasa ambapo ameeleza Mkoa kuwa na upungufu wa vyumba vya madarasa 7000 ,ambapo mwaka huu peke yake wanatarajia zaidi ya wanafunzi elfu 90 kuanza masomo.

"Ninawaomba wazazi wawapeleke watoto shule ,wasiwafiche na kuwatumikisha Shughuli za kilimo na kazi za ndani."Amesema Fatuma
Katibu tawala Mkoa wa Dodoma, Fatuma Mganga akizungumza na wandishi wa habari pamoja na maafisa Habari Mkoa wa Dodoma, Katika ukumbi wa kondoa irangi Wilayani Kondoa juu ya utekelezaji wa Program ya Serikali ya shule Bora 

Picha na Shakila Nyerere


Aidha amekemea dhana iliyozoeleka kwamba Mkoa wa Dodoma ni zao la wadada wa ndani  kutoa House girl[Wasaidizi wa Shughuli za ndani]

Amesema Mpaka kufikia January 26.2023 ilifikia asilimia  89.7 ya wanafunzi wa madarasa la awali walioripoti   shule,huku asilimia 94.2 Kwa darasa la kwanza na asilimia 66.95 kidato Cha kwanza


.."Nawaomba waandishi wa habari mkausaidie mkoa kutangaza mafanikio yaliyopatikana katika sekta ya elimu mkoani kwetu,kuyatangaza mafanikio haya Kwa jamii yatarahisisha serikali kuendelea kutuunga Mkono katika jitihada zetu hizi."Alisema Fatuma

Fatuma akapongeza kwa kusema juu ya Matamanio ya mkoa ya mwaka huu 2023 ni kuwa na ufaulu wa asili 95 ya matokeo ya mtihani wa darasa la saba na angalau asilimia 75 ya wanafunzi wanaohitimu kidato Cha Nne Wawe na ufaulu wa daraja la 1-3.

"Aidha ni matamanio ya mkoa kuondoa changamoto ya watoto kukaa chini Pamoja na wanafunzi wote watakaoshindwa mtihani wao wa darasa la saba kujiunga na vyuo vya ugundi stadi VETA"Amesema Fatuma

Naye mratibu wa Program ya shule Bora Mkoa wa Dodoma Mtemi Zombwe ametoa wito kwa wandishi kufanya kazi kwa kufuata Dira nne za Program zilizopo Katika shule Bora 

Hata hivyo alisema watoto wa darasa la kwanza na lapili ili waweze kufikia malengo ya kujua kusoma na kuandika inahitajika amani kwakua anakua Katika umri mdogo hivyo linalohitajika nikupewa amani
Waandishi wa habari, pamoja na maafisa Habari Mkoa wa Dodoma wakiwa makini kumsikiliza Katibu tawala Mkoa wa Dodoma Fatuma Mganga wakati akizungumza juu ya Program ya Serikali ya shule Bora

No comments: