Nehemiah Mchechu aliyeteuliwa kuwa Msajili wa Hazina |
Na Andrea Ngobole, Maipac
maipacarusha20@gmail.com
Rais Samia Suluh Hassan Amemteua Nehemiah Kyando Mchechu kuwa Msajili wa Hazina.
Katika taarifa kwa vyombo vya habari iliyotolewa jioni hii na kurugenzi ya mawasiliano Ikulu na kusainiwa na Mkurugenzi wa Mawasiliano Ikulu Zuhura Yunus imesema kuwa uteuzi huo unaanza Leo.
Kabla ya uteuzi huo Nehemiah Mchechu alikuwa Mkurugenzi Mkuu wa shirika la Nyumba la Taifa (NHC).
Mchechu anachukua nafasi ya Mgonya Benedicto ambaye atapangiwa kazi nyingine.
Rais pia amemteua Hamad Abdallah kuwa Mkurugenzi Mkuu wa shirika la Nyumba la Taifa (NHC) kabla ya uteuzi huo Hamad alikuwa Mkurugenzi mtendaji wa Gimcoafrica limited na anachukua nafasi ya Nehemiah Mchechu aliyeteuliwa kuwa Msajili wa Hazina.
Amemteua Mussa Mohamed Makame kuwa mkurugenzi mtendaji shirika la Maendeleo ya petrol Tanzania (TPDC).
Kabla ya uteuzi huo Makame alikuwa mjumbe wa bodi ya Wakurugenzi wa shirika la Maendeleo ya petrol Tanzania na pia ni mshauri mwelekezi wa masuala ya mafuta na gesi nchini Tanzania.
Makame anachukua nafasi ya Dkt.James Matagio ambaye atapangiwa kazi nyingine
Uteuzi huo ni kuanzia Leo tarehe 24/02/2023
No comments:
Post a Comment