👉Atoa wito kwa wananchi kuitumia
Na John Mapepele
maipacarusha20@gmail.com
Serikali imewataka wananchi wote nchini kutumia boti ya kisasa ya Utalii iliyozinduliwa rasmi leo ili kukuza utalii wa ndani.
Kauli hiyo ameitoa Waziri wa Maliasili na Utalii Mhe. Mohamed Mchengerwa Kilwa Masoko kwenye hafla ya uzinduzi wa boti maalum ya Utalii ijulikanayo kama TAWA SEA CRUISER inayomilikiwa na Mamlaka ya Usimamizi wa Wanyamapori Tanzania (TAWA).
Mhe. Mchengerwa amefafanua kuwa boti hiyo itakuwa ikifanya safari katika ukanda wote wa Pwani ili wajionee vivutio mbalimbali vya utalii.
Amevitaja baadhi ya vivutio vya utalii vinavyopatikana katika eneo la Kilwa kuwa ni pamoja na misitu ya matumbawe, kasa, mikoko, na samaki wa aina mbalimbali.
Katika hatua nyingine Mhe. Waziri ametembelea maeneo ya kitalii ya mji mkongwe wa kihistoria wa Kilwa na kujionea vivutio vya utalii vya asili kama msikiti wa Karne ya 12 magofu ya kale na jumba la mfalme.
Akiwa katika msikiti wa kale ameiagiza Bodi ya TAWA kuona namna ya kuboresha mji huo ili
kuvuta watalii wengi.
#tanzaniaunforgettable #tanzaniaroyaltour
No comments:
Post a Comment