SERIKALI YASEMA MATUMIZI YA TEHAMA KWENYE UHIFADHI NI JAMBO LISILOEPUKIKA - MAIPAC MEDIA TANZANIA

Breaking

MAIPAC MEDIA TANZANIA

A Centre for Indigenous and Pastoralists Community Informations




Thursday 13 April 2023

SERIKALI YASEMA MATUMIZI YA TEHAMA KWENYE UHIFADHI NI JAMBO LISILOEPUKIKA

  





Na: Mwandishi wetu

maipacarusha20@gmail.com

Serikali imesema matumizi ya TEHAMA  katika suala la ulinzi na usalama wa Maliasili ni suala lisiloepukika  huku ikisisitiza kuwa mfumo fungamanishi wa kieletoniki wa ufutiliaji matukio ya ujangili ni muhimu kwa mazingira ya Dunia ya sasa.


Mkurugenzi wa Mafunzo na Takwimu wa Maliasili na Utalii, Dkt. Edward Kohi  ametoa kauli hiyo leo Jumatano Aprili 12, 2023 Jijini Dodoma wakati akifungua Kikao kazi  kilichowakutanisha Wadau mbalimbali wa Uhifadhi  kwa ajili ya kuboresha na kudhibitisha nyaraka za mahitaji  ya mfumo fungamanishi wa kielektoniki utakaosaidia  katika ufuatiliaji wa matukio ya ujangili  na udhibiti wa maeneo yaliyohifadhiwa nchini


Amesema kuwa matukio ya ujangili wa wanyamapori na misitu yaliyokusanywa na Wataalamu ni sehemu ndogo tu ya mfumo mzima  wa kielektroniki wa uhifadhi utakaokuwa na mambo mengine fungamanishi  katika usimamizi na ufuatiliaji wa bioanuwai na matumizi ya maliasili.


Kufuatia hatua hiyo, Dkt.Kohi amewataka Wajumbe wa Kikao hicho kutumia weledi wao kutoa michango chanya na maoni ya kujenga yatakayosaidia kutengeneza mfumo  utakaosaidia Serikali katika masuala ya uhifadhi.


Ameongeza kuwa kukamilika kwa mfumo huo  kutasaidia  kupata tathmini na taarifa kwa usahihi na haraka  ili kurahisisha huduma za uhifadhi.


Kikao hicho kilichofadhiliwa na Mradi wa Kuzuia na  Kupambana na Ujangili wa Wanyamapori na Biashara haramu ya nyara na mazao ya Misitu ( IWT) mbali ya  kuwakutanisha Wadau wa Uhifadhi, pia kimewakutanisha  Wataalamu wa TEHAMA, Wataalamu wa Inteligensia  na Wakuu wa Idara na Vitengo

No comments: