WAZIRI MCHENGERWA : HAKUNA MUDA WA NYONGEZA MIRADI YA REGROW - MAIPAC MEDIA TANZANIA

Breaking

MAIPAC MEDIA TANZANIA

A Centre for Indigenous and Pastoralists Community Informations




Monday 17 April 2023

WAZIRI MCHENGERWA : HAKUNA MUDA WA NYONGEZA MIRADI YA REGROW

 

Waziri wa Maliasili na Utalii, Mohamed Mchengerwa akizungumza KATIKA hafla ya utiaji saini mikataba nane ya ujenzi WA majengo Utalii na viwanja vya ndege

Katibu Mkuu wa Wizara ya Maliasili na Utalii Dkt. Hassan Abbas akizungumza KATIKA hafla hiyo


Na: Pamela Mollel,Arusha

maipacarusha20@gmail.com

Waziri wa Maliasili na Utalii, Mohamed Mchengerwa amesema kuwa hakutakuwepo na muda wa nyongeza katika utekelezaji wa miradi nane ya REGROW yenye thamani ya sh, bilioni 157.2.


Akizungumza katika hafla ya utiaji saini wa mikataba nane ya ujenzi wa majengo ya utalii,ujenzi wa viwanja vya ndege aliisisitiza hatasita kuwachukuliwa hatua wakandarasi watakao zembea kumaliza  kazi kwa wakati  sahihi kwa kuwa miradi hiyo imechelewa sana kufanyikana kwa zaidi ya miaka minne sasa


Alisema viwanja sita vya ndege vitajegwa ikiwemo Hifadhi za Ruaha  viwanja vitatu,  Hifadhi ya Mwalimu Nyerere viwanja viwili na Hifadhi ya Mikumi kiwanja kimoja


Waziri aliongeza kuwa katika hifadhi ya Udzungwa itajengwa njia  njia ya juu ya utalii ya kilomita moja ambayo itakuwa njia ndefu katika njia zote Kusini mwa Afrika au Katika Nchi zaAfrika Mashariki.


Alitoa rai kwa wakazi wa mikoa ya kusini kuchangamkia fursa hivyo ya ujenzi wa miradi hiyo ili waweze kujipatia kipato 


Aidha aliwataka Shirika la hifadhi za Taifa Tanapa kukuza utalii Kusini mwa Tanzania  ili watanzania waone thamani ya miradi mbalimbali inayotekelezwa hapa nchini 


"Acheni ukiritimba lazima tubadilike miradi huu u

ulikuwa ufanyike mwaka 2019 mnapita huku mnaingia huku sasa hii si faida kwa nchi yetu, simamieni mikataba acheni ukiritimba katika utekelezaji wa miradi mbalimbali haiwezekani Rais Samia Hassan Suluhu aseme ameleta miradi Kusini halafu watu wanakwamisha hapa lazima tuhakikishe mambo yaliyokwama yanafanya kazi ndio maana tunakwamua mambo mbalimbali yaliyokwama "


Naye Katibu Mkuu waWizara hiyo,Dk, Hassan Abbas alisisitiza milango ya kufungua fursa za utalii Mikoa ya Kusini ifunguliwe ikiwemo kusaini mikataba hiyo nane kwaajili ya uboreshaji wa miundimbinu lengo ni kufungua fursa za utalii.


Alitoa onyo kali kwa maofisa manunuzi watakaokwamisha zoezi hilo kwa manufaa yao binafsi ili tu kukwamisha miradi hiyo kuwa atafute pa kwenda maana lengo la miradi ni kukamilika kwa wakati ili wafadhi ambao ni Benki ya dunia watoe mkopo mwingine





No comments: