MAJANGILI KUDHIBITIWA KIDIJITALI ENEO LA BURUNGE WMA - MAIPAC MEDIA TANZANIA

Breaking

MAIPAC MEDIA TANZANIA

A Centre for Indigenous and Pastoralists Community Informations




Saturday 20 May 2023

MAJANGILI KUDHIBITIWA KIDIJITALI ENEO LA BURUNGE WMA

Afisa wanyamapori  halmashauri ya wilaya ya babati Goodluck Kalambani




Na: Mwandishi wetu, Babati


maipacarusha20@gmail.com


Watuhumiwa wa ujangili katika eneo la ikolojia ya Hifadhi ya Taifa ya Tarangire na Manyara sasa wataanza kusakwa kupitia Mfumo maalum wa kidigitali unaotumika katika  kukusanya taarifa, zikiwepo picha, kuzihifadhi na kuzituma(SMART) kwa usahihi.


Mfumo huo wa kisasa utaanza kutumika mwaka huu, katika eneo la jumuiya ya hifadhi ya wanyamapori Burunge,kupitia mradi wa uhifadhi maliasili unaodhaminiwa na shirika la msaada la kimataifa la Marekani(USAID).


Akizungumza wakati akitoa mafunzo jinsi ya utumiaji wa mfumo, huo kwa askari wa wanyamapori wa Burunge WMA, askari wa halmashauri ya Babati na askari wa Mamlaka ya usimamizi wanyamapori(TAWA) Macarios Gisberth alisema mfumo huo utarahisha kuwadhibiti majangili kabla ya kuuwa wanyapori.


Gisberth ambaye ni afisa wa masuala ya Data, usomaji ramani na kuripoti kidigitali wa Taasisi ya Friedkin Conservation Fund, alisema mfumo huo ambao utatumia program maalum ambayo imewekwa katika simu za mkononi na kumpyuta, unaoweza wa kupiga picha, kutunza kumbukumbu ya eneo la tukio na kuzituma kwa uharaka.


"huu mfumo huu pia utawezesha kufanyika doria katika hifadhi za wanyamapori na kupata taarifa matukio ya ujangili kabla haujatendekeka, matukio ya uvamizi wa mifugo na uharibifu wa mazingira" alisema .


Afisa miradi wa tuhifadhi mazingira, ambao unaendeshwa na taasisi ya chemchem katika eneo la Burunge WMA, Martin Mng'on'go alisema katika mradi huo askari wanaofanyakazi katika eneo hilo, watakuwa wakitumia mfumo huo kukabiliana na ujangili.


"askari tayari wamejengewa uwezo kufanya doria kutumia mfumo wa SMART , kuwachunguza majangili na kuwakamata kirahisi zaidi"alisema


Afisa wa doria wa Mamlaka ya usimamizi wanyamapori (TAWA), Gabriel Charles alisema mfumo huo wa kisasa ni suluhu jinsi ya kukabiliana na majangili.

"tumeona jinsi mfumo huu,  utarahisha upangaji mzuri wa doria, kukusanya taarifa za uhalifu na kuzifanyia kazi"alisema


Afisa Wanyamapori wilaya ya Babati,Godluck Kalambani alisema mfumo huo utasaidia uchakataji wa taarifa na utoaji taarifa sahihi ikiwepo eneo ambalo mtumuhima ataonekana na hivyo kukamatwa kabla ya kutenda uhalifu.


Baadhi wa wahitimu wa mafunzo haya, Janet Gerald askari wa burunge WMA alisema mafunzo waliyopata yamekuwa na faida kubwa kwani sasa watatumia mfumo wa SMART kukabiliana na ujangili.


"tumefundishwa jinsi ya kutumia mfumo huu kupanga doria, kubainisha uvamizi eneo la hifadhi na kubaini eneo alipo jangili kwa  urahisi"alisema.


Katika eneo la Burunge WMA kumeibuka matukio ya ujangili wa Twiga mnyama wanyama ambao wapo wengi katika eneo hilo.

Mkufunzi Macarios Gisberth akiwafundisha maafisa wanyamapori na waongoza watalii matumizi ya Smart


No comments: