Dk Tulia apitishwa na Bunge la SADC kugombea Urais wa Umoja Mabunge Duniani - MAIPAC MEDIA TANZANIA

Breaking

MAIPAC MEDIA TANZANIA

A Centre for Indigenous and Pastoralists Community Informations




Friday, 7 July 2023

Dk Tulia apitishwa na Bunge la SADC kugombea Urais wa Umoja Mabunge Duniani


Dkt. Tulia Ackson akipongezwa baada ya kuchaguliwa



Na: Mwandishi wetu Arusha 


maipacarusha20@gmail.com


Spika wa Bunge la Tanzania, Dk Tulia Ackson, kapitishwa na Mabunge ya Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika(SADC),kugombea nafasi ya Rais wa Umoja wa Mabunge Duniani(IPU).


Uchaguzi  unatarajiwa kufanyika Octobar  27, mwaka huu nchini Angola.


Mbunge wa bunge la Afrika ya Kusini,Darren Bergman ndiye aliwasilisha hoja katika bunge hilo ,katika kikao cha 53 cha Jukwaa la Mabunge ya SADC kinachoendelea jijini Arusha na kuomba Mabunge yote kumuunga mkono Dk Tulia.


Amesema ametoa hoja ya  kupitishwa Dk Tulia  kuwania nafasi hiyo, kwa mujibu wa  kanuni ya 26(4) ya utaratibu katika bunge hilo.


Amesema amewasilisha hoja ya kupata mgombea mmoja kutoka SADC, licha ya kuwepo wagombea wengine walioonesha nia kugombea nafasi hiyo kutoka  Afrika.


Wagombea hao  ni Catherine Gotan Hara wa nchini Malawi na Jacob  Fransis Nzwidamilimo Mudenda wa Zimbabwe  na Adji Diarra Megane Kanoutee wa mbunge kutoka Senegal.


Bergman amesema ili kuonesha Umoja katika kuwania nafasi hiyo,ni vyema kumpitisha Dk Tulia Spika wa Bunge la Tanzania, kutokana na sifa  alizonazo kuwa mgombea wa SADC katika uchaguzi huo.



Hoja ya Mbunge huyo wa Afrika Kusini, iliungwa mkono na Mbunge kutoka nchini, Angola Pedro Sebastiano na kueleza kwa kuwa kwa muda mrefu nafasi hiyo, imekuwa ikishikwa na wabunge wanaume kumpitisha Dk Tulia ambaye ni msomi na kijana kuwania nafasi hiyo ushindi utapatikana.


"Naunga mkono hoja hii na ninawaomba wabunge wenzangu tuunge mkono,ili kuonesha umoja na mshikano ndani ya SADC hasa kuwa na mgombea mwanamke na ni kijana"amesema


Akizungumza baada ya kutolewa hoja hiyo, Rais wa Bunge la SADC,Roger Mancienne alitoa fursa ya wabunge kuchangia hoja hiyo, ambapo wabunge kutoka nchi za Zimbabwe, Jamuhuri ya Kidemokrasia ya Congo, Lesotho,Zambia,Eswatini Namibia, Afrika Kusini, Mauritania walieleza kumuunga mkono Dk Tulia.


Akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya kuchaguliwa kuwania nafasi hiyo, Dk Tulia aliwapongeza wabunge wote kwa kumpitisha na kuwania nafasi hiyo ya kuwa Rais wa Umoja wa Mabunge Duniani.


Amesema heshma aliyopewa ni kubwa kwani kuteuliwa kugombea nafasi hiyo katika bunge hilo lililoanzishwa tangu mwaka 1889 hadi sasa likiwa na wawakilishi wa mabunge 179 duniani.


Dk Tulia tayari amepitishwa pia na Bunge la Afrika(PAP) na Bunge la Jumuiya ya Afrika ya Mashariki (EALA) kuwania nafasi hiyo.


No comments: