Dkt. KIKWETE AVUTIWA NA MILA NA DESTURI ZA WAHADZABE - MAIPAC MEDIA TANZANIA

Breaking

MAIPAC MEDIA TANZANIA

A Centre for Indigenous and Pastoralists Community Informations




Wednesday, 12 July 2023

Dkt. KIKWETE AVUTIWA NA MILA NA DESTURI ZA WAHADZABE

 

RAIS WA awamu ya nne Dkt. Jakaya Kikwete na Mkewe Mama Salma Kikwete wakiwa na vijana WA jamii ya wahadzabe walipotembelea jamii hizo hivi karibuni

Dkt. Jakaya Kikwete na Mkewe Mama Salma Kikwete wakiwa na wamama WA kihadzabe walipitembea jamii hizo hivi karibuni 


Mke wa Rais Mstaafu Mama Salma Kikwete akiwa amembeba mtoto alipotembelea jamii ya Wahadzabe wanaoishi katika Kijiji cha Endamagha kilichopo Kata Tarafa ya Eyasi, Wilaya ya Karatu akiwa na Rais Mstaafu Dkt Jakaya Kikwete 



Na Mwandishi wetu KARATU

maipacarusha20@gmail.com


RAIS WA awamu ya nne Dkt.  Jakaya Kikwete na mkewe Mama Salma Kikwete wametembelea jamii ya Wahadzabe na kujifunza Mila na desturi zao za asili za kutafuta na kuhifadhi vyakula, malezi ya watoto na makazi yao. 


Pia walipata fursa ya kujifunza mambo mbalimbali ya mila za jamii hiyo inayoishi katika zama za kale za kula matunda na asali.


Pamoja na mambo mengine  waliweza pia kuongea kwa kina na jamii hiyo kuhusu changamoto zinazowakabili kama upatikanaji wa elimu kutokana na mfumo wao wa maisha wa kuhamahama, uvamizi wa makabila mengine katila maeneo yao ya asili hali inayotishia mtindo wao wa maisha pamoja na upatikanaji wa huduma nyingine muhimu za kijamii.

No comments: