Na Mwandishi Wetu,
maipacarusha20@gmail.com
Katibu Mkuu wa Wizara ya Maliasili na Utalii.Dk Hassan Abbas ameitaka taasisi ya Utafiti wa Wanyamapori nchini(TAWIRI) kutoa mbinu Bora zitakazowezesha uhifadhi na ustawi wanyamapori .
Akizungumza na menejimenti ya taasisi hiyo , Dkt. Abbas amesema kipaumbele cha Wizara ya Maliasili na Utalii ni kuendelea kuhifadhi maliasili iliyopo kwa kizazi hiki na kizazi kijacho.
Amesema sekta ya uhifadhi nchini inaitegemea TAWIRI kutoa mbinu bora zitakazo wezesha uhifadhi na ustawi wa wanyamapori na makazi yao.
Dkt. Abbas ametoa wito kwa Viongozi wa TAWIRI kuhakikisha umma unapata matokeo ya Tafiti za wanyamapori zinazofanyika ili kuzitumia kwa maendeleo.
Kwa upande wake Mkurugenzi Mkuu wa TAWIRI, Dkt. Ernest Mjingo amemshukuru Katibu Mkuu kwa ziara na nakuahidi kutekeleza maelekezo yote kwa manufa ya uhifadhi nchini.
No comments:
Post a Comment