ACER - AGA KHAN UNIVERSITY YASHAURI VIWANDA KUTUMIA NISAHATI SAFI ILI KUTOHARIBU MAZINGIRA - MAIPAC MEDIA TANZANIA

Breaking

MAIPAC MEDIA TANZANIA

A Centre for Indigenous and Pastoralists Community Informations




Thursday 18 July 2024

ACER - AGA KHAN UNIVERSITY YASHAURI VIWANDA KUTUMIA NISAHATI SAFI ILI KUTOHARIBU MAZINGIRA

Dkt. Emmanuel Sulle, Mkurugenzi wa Kituo cha utafiti wa masomo ya Tabianchi na mazingira cha chuo kikuu Cha Aga Khan kilichopo jijini Arusha akiwaeleza waandishi wa habari za mazingira namna kituo hicho cha utafiti kinavyofanya kazi kwa vitendo na kushirikiana na jamii inatozunguka huo hicho

 



Na Andrea Ngobole, maipac

 

Maipacarusha20@gmail.com

 

Kituo cha utafiti wa masomo ya Tabianchi na mazingira cha chuo kikuu Cha Aga Khan kilichopo jijini Arusha kimezishauri nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) kuongeza idadi ya viwanda vinavyozalisha bidhaa zisizoharibu mazingira na kufyonza kaboni kwa Maendeleo Endelevu (SDGs) ili kuwalinda binadamu, mimea na mifugo isipate madhara ya mabadiliko ya tabia nchi.

 

Mkurugenzi wa kituo hicho Dkt. Emmanuel Sulle ameyasema hayo katika ziara maalumu ya waandishi wa Habari za mazingira walipotembelea kituo hicho hivi karibuni kwa ajili ya kujifunza namna bora ya kutatua changamoto za athari za mabadiliko ya Tabianchi, uhifadhi bora wa mazingira na kudhibiti hewa ukaa.

 

Alisema endapo nchi za jumuiya ya Afrika mashariki zikiongeza zaidi viwanda vinavyozalisha bidhaa mbalimbali kwa kutumia nishati safi basi mazingira yatakuwa bora na wananchi watanufaika na ajira, utunzaji wa miti utakaowezesha uvunaji wa bayoanuwai na kufyonza kaboni ili kulinda mazingira.

 

Taasisi hiyo imejikita zaidi katika utafiti wa kutatua changamoto za mazingira kwa jamii kwa kuwawelimisha uzalishaji wa mazao mchanganyiko ili kufanikiwa kupata mazao na chakula cha kutosha kwa ajili ya familia na kuongeza kipato cha familia kwa kuuza mazao hayo.

 

“Elimu ya ukombozi nimuhimu sana kwa ajili ya kuleta mabadiliko ya Uchumi wa familia na jamii kwa ujumla” Alisema Dkt. Sulle

 

Amesema jamii zinazoishi ukanda wa Kaskazini mwa Tanzania ni jamii zinazoathiriwa na mabadiliko ya tabia nchi kutokana na ukame hivyo ni lazima wapande miti na majani yanayohimili ukame na upatikanaji wa malisho ili kuinua uchumi na kuondokana na changamoto za mmomonyoko wa udongo.

 

Alisema katika karne ya 21 elimu ya kukabiliana na mazingira na athari za mabadiliko ya tabianchi si ya kukaa darasani pekee lazima sasa wanafunzi watekeleze kwa vitendo ili kuhakikisha mazingira yanatunzwa ndio maana taasisi hiyo inashirikiana na jamii kwa kupata maarifa ya asili katika utunzaji wa mazingira ikiwemo mifugo.

 

"Katika taasisi hii tunayo miti zaidi ya 75 aina tofauti tofauti ikiwemo mti wa mpingo na tukiamua kuongeza viwanda lazima tujue vinazalisha bidhaa zisizo haribu mazingira lakini endapo ushirikishwaji wa utunzaji mazingira utashirikisha wanafunzi ngazi za chini utawasaidia kuwa mabalozi wa kuleta mabadiliko ya kweli" Alisema Dkt. Sulle

 

Alisema mabadiliko ya tabia nchi yanaleta athari kubwa kwa wananchi waliopo pembezoni hivyo kila mmoja anapaswa kulinda mazingira ili kuepukana na mabadiliko ya hali ya hewa na kuongeza kuwa mwaka huu nchi za Kenya na Tanzania zilipata athari ya mafuriko ya mvua kubwa kunyesha na kuharibu mazingira lakini sababu kubwa baadhi ya maeneo hayapo katika hali ya uhalisia kutokana na ukatwaji wa miti na udongo kutokana na shughuli za kibinadamu.

 

Alisisitiza upandaji wa miti zaidi katika maeneo mbalimbali ili kuvuta hewa nzuri na kuondoa magonjwa mbalimbali yanayotokana na mabadiliko ya hali ya hewa na kuachana na kilimo kisicho endelevu ikiwemo kutumia nishati mbadala kama vile gesi asilia inayopunguza uchafuzi wa mazingira ikiwemo matumizi ya sola.

 

Naye Mkurugenzi wa Kampasi ya Aga Khan Arusha, Murad Jivan alisema wanashirikiana na jamii katika kuhakikisha utunzaji wa mazingira ikiwemo upandaji wa miti, upandaji wa maua, kilimo cha majani kwaajili ya malisho ya mifugo ili kuwezesha wafugaji kuondokana na migogoro baina ya wakulima na wafugaji kutokana na ukosefu wa malisho unaosababishwa na shughuli za kibinadamu.

 


No comments: