MAMA NA BABA LISHE NAMTUMBO WAPATIWA MAJIKO YA NISHATI MBADALA - MAIPAC MEDIA TANZANIA

Breaking

MAIPAC MEDIA TANZANIA

A Centre for Indigenous and Pastoralists Community Informations




Friday 26 July 2024

MAMA NA BABA LISHE NAMTUMBO WAPATIWA MAJIKO YA NISHATI MBADALA

 

Mbunge wa Jimbo la Namtumbo  Vita Kawawa kulia akimkabidhi jiko la Gesi mmoja wa wanufaika


Mbunge wa Jimbo la Namtumbo  Vita Kawawa kulia akimkabidhi mmoja wa wanufaika wa majikonhayo


Na Mwandishi wetu,Namtumbo


maipacarusha20@gmail.com


MAJIKO ya nishati mbadala 300 yenye thamani ya sh 25.5 milioni yametolewa kwa wajasiriamali wadogo wanaotoa huduma ya chakula Mama na Baba lishe Wilaya ya Namtumbo mkoani Ruvuma.


Mbunge wa Jimbo la Namtumbo  Vita Kawawa amesema kutolewa kwa majiko hayo ni ili waweze kutumia nishati safi  na kuondokana na ugonjwa wa kukosa pumzi na vifo vinavyotokana na kuvuta moshi wenye sumu


Akizungumza na wajasiliamali hao jana wakati wa hafla fupi ya ugawaji wa majiko hayo ambayo ni msaada kutoka kwa Rais Dk Samia Suluhu Hassan mbunge Kawawa alisema wabunge kila mara wamekuwa wakipiga kelele ya kuomba bei ya gesi kushuka ili kila mwananchi aweze kutumia nishati safi na Salama ya kupikia na kuondokana na matumizi ya mkaa na kuni.


Naye Mkurugenzi wa kampuni ORYX Peter Ndomba alisema kila mwaka watu 33,000 ufariki dunia kutokana na kuvuta moshi wenye sumu hivyo aliwashauri wananchi kutumia nishati safi ya kupikia kwa ajili ya afya zao.


Nao Wajasiriamali hao akiwemo  Tugonze Pawa na Sophia Hamis walisema kuwa wamepokea majiko hayo lakini ombi lao kubwa kwa serikali ni kupunguzwa kwa gharama za ujazaji wa gasi ili iendelee kuwa msaada kwao .


Mwisho.

No comments: