Stesheni masta msaidizi Morogoro Godfrey Temba |
Na: Lilian Kasenene, Morogoro
maipacarusha20@gmail.com
MABEHEWA matano kati ya 20 ya Treni ya Mizigo iliyokuwa kwenye Reli ya Kati ikitokea jijini Dar es salaam kuelekea Mikoa ya bara yameanguka eneo la Bingwa kwa Masista Manispaa ya Morogoro.
Akizungumza na Waandishi wa Habari, Stesheni masta msaidizi Morogoro Godfrey Temba alisema treni hiyo ilibeba mzigo wa ngano na ilikuwa na mabehewa 20 ambapo kati ya hizo mabehewa matano yamepinduka.
Temba alisema ajali imetokea saa 12 jioni na bado chanzo Cha ajali hiyo hakijafahamika kwa sasa mafundi wanaendelea na uchunguzi kubaini chanzo chake lakini hakuna madhara yoyote ya kibinadamu yaliyojitokeza.
Mwisho.
No comments:
Post a Comment