Mahakama ya Mbulu yashindwa Kutoa Hukumu dhidi ya Mchungaji Aliyemlawiti Mtoto - MAIPAC MEDIA TANZANIA

Breaking

MAIPAC MEDIA TANZANIA

A Centre for Indigenous and Pastoralists Community Informations




Friday 23 August 2024

Mahakama ya Mbulu yashindwa Kutoa Hukumu dhidi ya Mchungaji Aliyemlawiti Mtoto





Na: Epifania Magingo, Babati 


maipacarusha20@gmail.com 


Mahakama ya Wilaya ya  Mbulu Mkoani Manyara imeshindwa kutoa hukumu dhidi ya Mchungaji wa mifugo Carol Christopher (18) mkazi wa Kijiji cha Moringe Kata ya Daudi anaekabiliwa na shtaka moja la kumlawiti mtoto mwenye umri wa miaka miwili na miezi tisa baada ya kushindwa kufika kusikiliza hukumu yake iliyopangwa kutolewa agosti 21 mwaka huu.


Upande wa mashtaka safari hii ukiongozwa na mwendesha mashtaka mkaguzi wa polisi maraba masheku badala ya mwendesha mashtaka katika shauri hilo kiongozi mkaguzi wa polisi wakili Hamilton Mosses ameiomba Mahakama hiyo kuwa ipo tayari kwa mshtakiwa kusikiliza matokeo ya shauri lake linalomkabili.


Lakini  mama wa mshtakiwa Carol, Anna Burra ambaye amemuwekea dhamana kijana wake ameiambia mahakama hiyo kuwa mshtakiwa ameshindwa kufika kusikiliza hukumu dhidi yake  baada ya kusumbuliwa ugonjwa wa tumbo la kuhara na hivyo amelazwa katika Hospitali ya Seriani Mkoani Arusha  hivyo na kwamba anamleta  mahakamani hapo  agosti 26 kama ilivoamriwa amri na mahakama.


 Mdhamini Anna Burra ameelezwa kuwa  hakuonyesha kielelezo chochote  aidha pia kutoulizwa kuonyesha kielelezo cha vyeti vinavyothibitisha  kuugua kwa mashtakiwa carol  mbele ya meza ya hukumu ya  Hakimu  Mkazi Mwandamizi Mfawidhi  Johari Kijuwile wa Mahakama hiyo huku  mdhamini huyo alisisitiza kuwa alilazwa tangu agosti 19 mwaka huu.


Kwa upande mwingine  Hakimu kijuwile alipotaka kufahamu atapewa ruksa lini ili mahakama hiyo iweze kutoa maamuzi, Mdhamini Anna Burra  ameiambia mahakama hiyo kuwa kwakuwa hali ya mshtakiwa sio mbaya ataweza kufika baada ya siku tatu.


Hata hivyo Hakimu kijowile amemuamuru mdhamini Anna Burra  kutii amri ya Mahakama anahakikisha anamfikisha mshakiwa Carol Christopher agosti 26 majira ya saa 3:00 asubuhi akiwa na vielelezo vya Hospitali ya Selian vinavyothibitisha mshtakiwa alikuwa amelazwa na kupatiwa matibabu kwenye hospitai hiyo.


Shauri hilo limefikia tamati baada ya upande wa utetezi katika mahakama hiyo kufunga utetezi uliowasilisha mashahidi watatu ambao pia walionekana kuwa waongo huku upande wa mashtaka kuwasilisha mashahidi sita’


Awali,Mwendesha Mashtaka katika shauri hilo Kiongozi Mkaguzi wa Polisi Wakili Hamilton Mosses akisoma hati ya mashtaka alisema Mshtakiwa Carol Christopher (18) amesema mnamo juni 13 majira ya saa tisa alasiri katika Kitongoji cha Getagu   alimwingilia isivyo halali na bila ya ridhaa yake mtoto mwenye umri wa miaka miwili na miezi tisa na kisha kumlawiti katika eneo la malisho alikokuwa akichunga ng’ombe na hivyo kukamatwa.

No comments: