Na Epifania Magingo, Babati
maipacarusha20@gmail.com
Kuelekea Uchaguzi wa Viongozi wa Serikali za mitaa ambao utakaofanyika 27 Novemba 2024,Mkuu wa Wilaya ya Hanang' Mkoani Manyara Almish Hazali à metoa rai kwa wananchi kujitokeza kwa wingi na kushiriki kikamilifu kupiga kura ili kupata kiongozi bora na mwenye nia ya maendeleo.
Akizungumza mara baada ya ibada ya Uzinduzi wa Kanisa la Elim Pentekoste Tanzania,Kata ya Jorodom Wilaya ya Hanang, kiongozi huyo amesema ni kila mwananchi anahaki ya kumchagua kiongozi ambae anaona ana uwezo wa kuleta mabadiliko chanya katika jamii na Taifa kwa ujumla.
Aidha, Almish amewatoa hofu wakazi wa Wilaya ya Hanang' na kusema kuwa uchaguzi huo utafanyika kwa amani na utulivu kwakuwa ulinzi na usalamà umezidi kuimarishwa katika wilaya ya hiyo.
"Wilaya yetu ya Hanang,Ipo Shwari naomba wananchi wote wa Hanang Tuwe na Amani Maeneo Yote,maneno mnayosikia ni Maneno ya mtaani lakini Serikali muda wote ipo na ninyi wananchi wake"Amesema Almish
"Tumeona taarifa kwenye vyombo vya habari watoto wanapotea kwa mazingira ya utatanishi, kwa kweli hatuna amani ila kwa sababu mkuu wa wilaya ametuambia kuwa kuna ulinzi, tunaomba uendele uimarishwe hasa maeneo yetu hayà ya vijijini"Alisema Selina Sixtbet Mkazi wa wilaya Ya Hanang
Kwa Upande wake Askofu Mkuu wa Kanisa la Elim Pentekoste Tanzania Askofu Peter Konki akizungumza wakati wa kuweka wakfu Jengo la Kanisa la Elim Pentekoste Jorodom amewatahadharisha wananchi kuwa makini dhidi ya viongozi wanaowarubuni kwa zawadi ili waweze kuingia madarakani.
"Kuuza Kura ni Kujinyima haki ya msingi,Kila mmoja aende apige kura na kumchagua kuongozi sahihi,kura ni Maamuzi kuuza kura ni kijinyima maamuzi na kuweka kichwa chako kwenye mfuko wa mwenye Elfu Tano, Jambo hili Halikubaliki"Amesema konki
Hata hivyo baadhi ya wananchi wamekiri kujawa na hofu Kutokana na uwepo wa taarifa za hivi karibuni za matukio ya watoto,kuuwawa na kutolewa Figo.
No comments:
Post a Comment