Madiwani Wa jiji la Arusha waapishwa, Meya Maximilian atetea Kiti chake - MAIPAC MEDIA TANZANIA

Breaking

MAIPAC MEDIA TANZANIA

A Centre for Indigenous and Pastoralists Community Informations




Thursday, 4 December 2025

Madiwani Wa jiji la Arusha waapishwa, Meya Maximilian atetea Kiti chake

 






Na Queen Lema Arusha 


maipacarusha@gmail.com


Madiwani 34 kutoka jiji la Arusha wameapishwa rasmi  Leo pamoja na kumpitisha Kwa kishindo aliyekuwa meya wa jiji Hilo, Maximilian Iranqhe Kwa Kura 33 na hivyo  kuendelea kuongoza baraza Hilo 2025_2030


Akiongea Leo  mara baada ya kutangazwa rasmi Meya Maximilian Alisema kuwa bado ana kazi kubwa ya kufanya ndani ya jiji la Arusha 


Alisema kuwa Kwa kipindi kilichopita waliweza kufanya kazi nyingi sana za maendeleo lakini pia kufanya kazi kama kiongozi Wa serikali za mitaa ndani na nje ya nchi 


Alifafanua kuwa Kwa kipindi kilichopita waliweza kutekeleza miradi mbalimbali lakini bado Ipo ambayo haijalamilika hivyo Kwa kipindi hiki cha Miaka mitano watahakikisha kuwa wameweza kutekeleza miradi hiyo 


"Kuna miradi mbalimbali kama ya  barabara  ambayo inaitaji nguvu ya pamoja katika Baraza hili jipya tutahakikisha kuwa tumeyatekeleza yote"aliongeza


Alihitimisha kwa kuwataka madiwani wote kuhakikisha wanafanya kazi kwa ufanisi mkubwa ikiwa ni pamoja na kutatua changamoto mbalimbali za wananchi Kwa ujumla


Wakati huo huo mgombea  nafasi ya unaibu Meya ,Calling Nathani ,pamoja na Julius ole Sakeyani waliomba kura kwa wmadiwani huku Mshindi akiwa ni Julius ole Sakeyani


Naye Julius Sakeyani ambaye alipata Kura 31 akiongea mara baada ya kushinda kiti hicho alisema kuwa kwa sasa kazi yake kubwa ni kuhakikisha kuwa anamsaidia mheshimiwa Meya.


Sakeyani alisema kuwa atahakikisha kuwa anasimamia vyema nafasi yake lakini ili aweze kutekeleza hayo anaitaji ushirikiano mkubwa Baina ya madiwani ,Meya , pamoja na halmashauri Kwa pamoja

No comments: