MKOA WA PWANI WATOA TUZO KWA TANROAD PWANI - MAIPAC MEDIA TANZANIA

Breaking

MAIPAC MEDIA TANZANIA

A Centre for Indigenous and Pastoralists Community Informations




Thursday, 11 December 2025

MKOA WA PWANI WATOA TUZO KWA TANROAD PWANI

 




Na Julieth Mkireri,MAIPAC KIBAHA


maipacarusha@gmail.com


OFISI ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani imemkabidhi Tuzo ya utendaji bora wa kazi Meneja wa Wakala wa Barabara wa mkoa huo Baraka Mwambage.


Akikabidhi tuzo hiyo Mkuu wa Mkoa wa Pwani Abubakar Kunenge amesema Meneja Mwambage amekuwa akifanya kazi kwa bidii jambo lililopelekea ofisi yake kutoa tuzo hiyo.


Amesema ofisi yake imekuwa ikitoa barua za kutambua kazi nzuri za viongozi kwenye Wilaya na kwa awamu hii ni mara ya kwanza kutoa tuzo ya kutambua utendaji bora wa kiongozi wa Tasia ya Tanroads.


Kunenge amesema utoaji wa tuzo utakuwa endelevu kwa watumishi watakaokuwa wanafanya kazi kwa bidii kutatua changamoto za wananchi.


Mhandisi Mwambage ameishukuru ofisi ya Mkuu wa Mkoa kwa kutambua kazi yake huku akiahidi kuendelea kutoa ushirikiano kufikia malengo yaliyowekwa katika taasisi yake.


Mwisho.

No comments: