Dkt Samia: Amani ni hazina yetu kiuchumi, kijamii - MAIPAC MEDIA TANZANIA

Breaking

MAIPAC MEDIA TANZANIA

A Centre for Indigenous and Pastoralists Community Informations




Tuesday, 21 April 2026

Dkt Samia: Amani ni hazina yetu kiuchumi, kijamii

 

Rais wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan







Na Mwandishi Wetu 


maipacarusha20@gmail.com 


Rais wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan amesema amani iliyopo nchini ni hazina ya shughuli za kiuchumi na kijamii.


Dkt Samia amesisitiza kuwa bila amani, hakuna kujenga uchumi wala hakuna shughuli za kijamii.


Ametoa kauli hiyo leo tarehe 21 Aprili, 2026 katika kongamano la mama na baba lishe lililofanyika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNICC), Jijini Dar es Salaam, 


“Mmeshuhudia siku tatu zile, hakukuwa na kuchezana, hakuwa na harusi wala ‘kitchen party’, hakukuwa na mimina wala mkusanyiko kwenye bar. Hakukuwa na chochote zilikuwa siku tatu tu...,” amesema Dkt Samia.


Mkuu huyo wa nchi, ametumia jukwaa la kongamano hilo,kuwaomba Watanzania kueindeleza amani ya Taifa.

No comments: