Wanahabari wapewe uhuru ili wawe wabunifu kwenye kazi zao - MAIPAC MEDIA TANZANIA

Breaking

MAIPAC MEDIA TANZANIA

A Centre for Indigenous and Pastoralists Community Informations




Wednesday, 29 April 2026

Wanahabari wapewe uhuru ili wawe wabunifu kwenye kazi zao

 

Wakili Dkt. Anna Henga mkurugenzi wa kituo cha kisheria na haki za binadamu (LHRC



 


 

Na Queen Lema,Arusha


maipacarusha20@gmail.com 


Imeelezwa kuwa  ili wana habari waweze kuwa wabunifu kwenye kazi zao wanatakiwa kupewa uhuru mzuri wa kufanya kazi zao 


Ukosefu wa uhuru kwa vyombo vya habari hapa nchini umesababisha baadhi ya waandishi kukosa uhuru wa kufanya kazi zao 


Hayo yameelezwa na Dkt. Anna Henga ambaye ni mkurugenzi wa kituo cha kisheria na haki za binadamu (LHRC) wakati akiongea kwenye mjadala wa uhuru wa vyombo vya habar ambao unaendelea Jijini Arusha 


Mkurugenzi huyo alisema  kuwa kwa sasa kuna baadhi ya vyombo vya habari ambavyo vimeshindwa kufanya kazi zao kwa weledi kwa kuwa kuna vitisho ambavyo vinasababisha ubunifu kukosekana kitu ambacho kinasababisha walaji wa habari kukosa vitu muhimu kwenye habari


Alisema kuwa Serikali inatakiwa kuhakikisha kuwa inawapa uhuru wa kutosha kwa vyombo vya habari lakini pia wakubali  kukosolewa lakini pia wanahabari wanapokosea pia wapewe nafasi ya kusikilizwa.


"Pamoja na kwamba wana habari wameminywa serikali inapaswa kuwapa nafasi hata kama wamekosea ikiwa ni pamoja na kuwaita na kuwasikiliza na sisi tunaamini kuwa kama watafanya ivyo ubunifu utakuwa ni mkubwa sana"aliongeza


Nao waandishi wa habari walioshiriki katika mjadala wa siku ya maadhimisho ya uhuru wa vya habari walisema kuwa wakati mwingine muingiliano wa sera unasababisha washindwe kuwajibika vyema kwenye utendaji kazi wao


Mmoja wa waandishi hao Bertha  Ismaili alisema kuwa wakati mwingine wanashindwa kufichua baadhi ya mambo kutokana na kuwepo kwa mazingira ambayo sio rafiki baina ya Serikali,wamiliki 


Alihitimisha kwa kuomba kuwepo  kwa uwazi mzuri lakini pia kuwezeshwa kwa kila namna kufanikisha maitaji yanayoitajika ili jamii iweze kupata chakula cha habari.


Mwisho

No comments: