Dkt. Lukumayi aomba Maliasili na Utalii kuongeza kiwango Cha miradi - MAIPAC MEDIA TANZANIA

Breaking

MAIPAC MEDIA TANZANIA

A Centre for Indigenous and Pastoralists Community Informations




Wednesday, 13 May 2026

Dkt. Lukumayi aomba Maliasili na Utalii kuongeza kiwango Cha miradi

 





Na mwandishi wetu,Dodoma


maipacarusha20@gmail.com 


Mbunge wa Jimbo la Arumeru Magharibi Dkt Johannes Lukumayi ameomba wizara ya Mali asili na utalii kuongeza kiwango Cha miradi mbalimbali katika vijiji na kata ambazo zimepakana na vivutio vya utalii, katika Jimbo lake.


Mbunge huyo akiwasilisha ombi Hilo juzi kwa Naibu waziri wa Mali asili na utalii Hamad Chande, mbunge huyo alisema kuwa Bado vijiji vilivyopakana na maeneo ya vivutio Kuna changamoto mbalimbali ikiwemo uwepo na  miradi michache 


Dkt Lukumayi alisema kuwa  wananchi wanaozunguka katika vivutio vya utalii wanatakiwa kuwa namba Moja kunufaika na vivutio hivyo 


Aliongeza kuwa vivutio hivyo kama vile hifadhi ya msitu wa Meru,pamoja na hifadhi ya Arusha


Alisema kuwa ni wakati muafaka sasa kwa Serikali kuangalia namna ya kurudisha fadhila kwa wananchi wanaozunguka vijiji  vya vivutio hivyo 


Dkt Lukumayi aliainisha kata na vijiji vinavyopakana na hifadhi ya msitu wa Meru -Usa ni pamoja na kata ya Oldonyosambu,Kata ya Olmtonyi,kata ya Kimunyaki  pamoja na Kiutu 


" Tunaomba Wizara kwa kushirikiana na Serikali sasa waweze kutusaidia katika miradi mbalimbali pamoja na kutatua changamoto zilizopo kama sehemu ya faida kwa jamii kwa kuwa wananchi wanatakiwa Kuona umuimu wa vivutio hivyo"aliongeza.


Kwa upande wake Naibu waziri wa maliasili na utalii,Hamad chande alisema kuwa amelichukua jambo Hilo na atalifanyia kazi ombi Hilo la Mbunge huyo ambaye amewasilisha .


Mwisho

No comments: