Nchi za Afrika zatakiwa kufuata Sheria na kulinda haki za binadamu. - MAIPAC MEDIA TANZANIA

Breaking

MAIPAC MEDIA TANZANIA

A Centre for Indigenous and Pastoralists Community Informations




Thursday, 7 May 2026

Nchi za Afrika zatakiwa kufuata Sheria na kulinda haki za binadamu.

 

Raisi wa TLS wakili Boniface Mwabukusi


Na Queen Lema Arusha 


maipacarusha20@gmail.com 


Chama Cha wanasheria wa Afrika(PALU)kimesema Kuna umuimu wa Sheria kufuatwa na kuzingatiwa ipasavyo pamoja na kulinda Haki za binadamu hasa kwa nchi za Afrika.


Hayo yameelezwa na Ofisa mtendaji wa PALU, Donald Deya wakati akifungua mkutano mkuu wa chama Cha wanasheria Tanganyika (Tls) Arusha.


Alisema kuwa Haki za binadamu zinatakuwa kulindwa ipasavyo na kuheshimiwa hivyo jamii inapaswa kujua na kutambua kuwa Hilo linatakiwa kutekelezwa vyema.


" Ninyi vyama vya kisheria mnatakiwa kujua na kutambua kuwa mna wajibu wa kusimamia Sheria pamoja na haki ipasavyo msikubali Kuona haki za binadamu zikiwa zinavunjwa alafu mnakaa kimya kwa kweli ni mbaya sana 


Na pia hata Tls nanyi pia muendelee kujitokeza kusimamia utawala wa Sheria kila maali mnapoona hapaendi sawa Hapo mtakuwa mmesaidia jamii yenu na bara letu kwa ujumla"aliongeza


Naye Raisi wa TLS wakili Boniface Mwabukusi alisema kuwa chama chake bado kipo kwenye mstari wa kuhakikisha kuwa Sheria inasimamiwa ipasavyo ikiwa ni pamoja na kutekeleza wajibu kwa mujibu wa taaluma 


Mwabukusi alisema kuwa hawauzi wajibu wa kisheria Bali wanatekeleza na ni kwa maslai ya jamii


Wakati huo huo wakili Mwabukusi amelitaka Jeshi la polisi nchini kuhakikisha kuwa watuhumiwa wanaokamatwa hawakaii nao sana Bali wafikishwe katika ngazi ya mahakama ili Hali iweze kutendeka.


Alihitimisha kwa kuwataka mawakili kusimamia ipasavyo maadili yao ya kazi pamoja na kutekeleza ipasavyo wajibu wao kwani kwa sasa TLS haitawafumbia macho wasio kuwa na maadili


Mwisho

No comments: