Na Mwandishi wetu..Aruaha
maipacarusha20@gmail.com
Chuo cha uhasibu Arusha kinatarajia kukutanisha wadau mbali mbali wa sekta utalii kutoka ndani na nje ya nchi katika kongamano la utalii la kimataifa litakalofanyika September 24 mwaka huu ikiwa ni fursa ya kutangaza nchi kwenye sekta ya utalii.
![]() |
Akizungumza katika ufunguzi wa maandalizi ya kongamano hilo, uliofanyika katika chuo cha Uhasibu Arusha naibu mkuu wa chuo upande wa taaluma ,tafiti na ushauri wa kitaallam chuo cha uhasibu Arusha dkt Grace Temba alisema kuwa wameanza maandalizi mapema kwani ni la muhimu sana kwa wadau wote wa utalii
Alisema kuwa wanatarajia kongamano la mwaka ambalo ni la nne kufanyika chuoni hapo linakutanisha wadau mbali mbali wa sekta ya utalii kutoka hapa nchini na nje ya Tanzania pamoja na kimataifa na kwamba ni la muhimu sana kwa taasisi hiyo wadau pamoja na serikali.
" katika kongamano letu hili tunatarajia kukutanisha watunga sera wa taaaisi na watafiti wa sekta ya utalii pamoja na wadau ambao watasaidia kutoa maboresho ya sekta ya utalii ambayo yatanufaisha pande zote lakini na chuo chetu kitatoa tafiti zake"aliongeza
Naye kaimu mkuu wa kitivo jinsia na sayansi ya jamii Lorna Mwijarubi alieleza kuwa mwitikio wa konhamano hilo ni mkubwa kwani wamepata mafanikio makubwa ikiwemo wadau kuwapatia wanafunzi wa chuo hicho naffasi ya mafunzo ya vitendo ambayo yamewawezesha kujifunza mambo ya utalii na ukarimu.
Alisema katika kongamano hilo wanatarajia kupata ubunifu na tafiti mbali mbali ambazo zitawezesha kuongeza uzoefu kwenye utalii.
Joaiven Karama ni Mwanafunzi wa mwaka wa pili katika chuo cha uhasibu Arusha alisema kongamano hilo ambalo ni la mara ya nne limewasaidia kutambulisha kozi ya utalii na ukarimu inayofundishwa chuoni hapo pamoja na kupata uwanda mkubwa wa kukutana na wadau wa utalii ambao wamewaongezea uzoefu.




No comments:
Post a Comment