WANAFUNZI 1000 WENYE MAHITAJI MAALUM DODOMA WAPEWA VIFAA VYA MILION 32 NA MBUNGE VITI MALUMU. - MAIPAC MEDIA TANZANIA

Breaking

MAIPAC MEDIA TANZANIA

A Centre for Indigenous and Pastoralists Community Informations




Sunday, 29 January 2023

WANAFUNZI 1000 WENYE MAHITAJI MAALUM DODOMA WAPEWA VIFAA VYA MILION 32 NA MBUNGE VITI MALUMU.

 

Mbunge viti malum Mkoa wa Dodoma,Marium Ditopile akiwa na wanafunzi alupowatembelea kwa kuwapatia vifaa mbalimbali vya shule. 

Picha na Shakila Nyerere

Mbunge wa jimbo la Mvumi Livingston Lusinde mwenye Shati ya blue pamoja na Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Dodoma Mjini Charles Mamba mwenye Suti katikati wakimsapoti kuonesha vifaa Mbunge Viti Maalum Mkoa wa Dodoma Marium Ditopile mara baada ya kuzungumza na wandishi wa habari

Picha na Shakila Nyerere

Na Shakila Nyerere, Maipac


MBUNGE viti Maalum Mkoa wa Dodoma anayetokana na Jumuiya ya Wanawake Tanzania (UWT)  Mariam Ditopile amewawezesha wanafunzi wenye Mahitaji Maalumu vifaa vya shule  kwa wanafuzi 1000 vyenye thamani ya zaidi  ya shilingi Milioni 30.

Akiongea na waandishi wa habari mara baada ya kukabidhi vifaa hivyo kwa wilaya zote saba za Mkoa wa  Dodoma, Ditopile amesema amefanya hivyo ikiwa ni kuunga mkono juhudi za Mheshimiwa Rais na pia kusherehekea kumbukizi ya  Kuzaliwa Rais  Samia  Suluhu Hassani.

Aidha Amewaomba Wadau Mbalimbali  Nchini Kutoa Kipaumbele Zaidi Katika Sekta ya Elimu kwa kutoa misaada hasa kwa Watoto yatima na wenye Mazingira Magumu yatakayo sababisha Kukatisha Masomo na kupoteza Ndoto zao Katika kupata elimu Bora

Naye Mwanaisha Juma Mwanafunzi wa kidato Cha tatu Katika shule ya Kwapakacha wilayani Kondoa  ametoa shukrani Kwa niaba ya wenzake  kwa msaada huo nakumuombea Dua Mh Marium Ditopile kwa namna alivyoguswa Katika suala Zima la kuigusa Elimu

No comments: