NA: ANDREA NGOBOLE, MAIPAC
maipacarusha20@gmail.com
Rais Dkt. Samia Suluh Hassan amefanya uteuzi wa Waziri, NaibuWaziri, Wakuu wa Mikoa, Makatibu Wakuu na Manaibu Makatibu wakuu pia kuwahamisha wizara baadhi ya Manaibu mawaziri na kuwatengua baadhi ya mawaziri na Mkuu wa mkoa.
kwa mujibu wa taarifa ya IKULU iliyotolewa leo jumapili na kusainiwa na Katibu Mkuu Kiongozi, Dkt.Mosses M. Kusiluka imesema kuwa Mheshimiwa Abdallah Hamis Ulega ameteuliwa kuwa Waziri wa Mifugo na Uvuvi na kuchukua nafasi ya Mashimba Ndaki ambaye uteuzi wake umetenguliwa.
Kabla ya hapo Mheshimiwa Ulega alikuwa naibu Waziri katika Wizara hiyo ya Mifugo na Uvuvi.
Mheshimiwa Hamisi Mohamed Mwinjuma akila kiapo cha utiifu Bungeni jijini Dodoma ambaye leo ameteuliwa na Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluh Hassan kuwa Naibu Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo |
Taarifa imesema kuwa Mheshimiwa Hamisi Mohamed Mwinjuma ameteuliwa kuwa Naibu waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo kuchukua nafasi ya Pauline Gekul ambaye amehamishiwa kuwa Naibu Waziri wa Katiba na Sheria.
kwa taarifa zaidi za wateule wengine soma hapa chini katika taarifa rasmi ya IKULU.
No comments:
Post a Comment