NAIBU
Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mheshimiwa Ridhiwani Kikwete akizungumza na wakazi wa Chamakweza
NAIBU
Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mheshimiwa Ridhiwani Kikwete akisalimiana na wakazi wa Chamakweza |
NA:JULIETH MKIRERI, MAIPAC CHALINZE
maipacarusha20@gmail.com
NAIBU
Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mheshimiwa Ridhiwani Kikwete ametoa
maagizo kwa wakazi wa Kijiji cha Chamakweza Kata ya Vigwaza kukaa
pamoja na kutatua migogoro yao kabla hatua nyingine hazijachukuliwa.
Kikwete
ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Chalinze alitoa maagizo hayo juzi
alipokutana na wananchi hao katika ziara yake ya kusikiliza kero za
wananchi ambapo katika kijiji hicho upo mgogoro wa muda mrefu kati ya
wakulima na wafugaji.
Akizungumza
katika mkutano huo amesema Chamakweza kumekuwa na mambo ambayo hayaendi
sawa kwa muda mrefu kati ya jamii mbili za wakulima na wafugaji hali
inayochangia baadhi ya mipango ya maendeleo kushindwa kufanyika kama
ilivyopangwa.
" Wazee
kaeni tafuteni suluhu ya migogoro mliyo nayo kama mmeshindwa kutafuta
amani yenu wenyewe niambieni nitawaonyesha inavyopatikana, nitarudi hapa
Machi katikati nikute matatizo yamemalizika tujadili mengine" amesema.
Kikwete
amesema wananchi hao kabla ya kuikaribisha serikali kuingilia migogoro
yao wanatakiwa kuitatua wenyewe kwa kufanya vikao vitakavyowahusisha
wazee katika kutafuta suluhu.
Amesema
mgogoro wa mpaka uliopo kati ya Chamakweza na Pingo hauwezi kutatuliwa
iwapo wenyeji wa Chamakweza wenyewe kwa wenyewe hawaelewani kwa kila
mmoja kusimamia uhalali wake wa kuishi katika eneo hilo huku kukiwa na
migongano ya kila siku inayokwamisha maendeleo.
Katika
hatua nyingine Kikwete amesema Serikali imebaini uwepo wa migogoro
mingi ya ardhi na hivyo inatarajia kupima na kutoa hati miliki za ardhi
katika mikoa yote hapa nchini.
Kwa
mujibu wa Kikwete katika utekelezaji huo Serikali imetenga zaidi ya
Bilioni 300 lengo likiwa ni kuondoa migogoro ya ardhi iliyokithiri katika
maeneo mbalimbali ambayo imekuwa kikwazo cha kufikia malengo ya
maendeleo yanayopangwa.
Awali
akizungumza katika mkutano huo Diwani wa Vigwaza Mussa Gama amesema
kijiji cha Vigwaza kinakabiliwa na vikwazo vya maji na mgogoro wa mpaka.
No comments:
Post a Comment