Mbunge wa jimbo la Chalinze Ridhiwani Kikwete akizungumza na walimu pamoja na wazazi wa wanafunzi wa shule ya sekondari ya Kikaro |
Mbunge wa jimbo la Chalinze Ridhiwani Kikwete akikata utepe shule ya sekondari kikaro |
Na JULIETH MKRERI,MAIPAC CHALINZE
maipacarusha20@gmail.com
MBUNGE wa Chalinze Ridhiwani Kikwete amewataka wanafunzi wanaomaliza kudato Cha SITA kuepuka tamaa za Dunia na kujali masomo Yao kwanza.
ameyasema hayo aliposhiriki sherehe za kuwaaga wanafunzi wanaomaliza kidato cha sita katika shule ya sekondari ya Kikaro Kata ya Miono wilayani Chalinze.
Katika sherehe hizo Mbunge huyo amewaasa wanafunzi hao kuepuka tamaa za dunia na kujali masomo kwanza kwa kuendelea na Elimu ya juu ili watimize malengo Yao.
Katika hatua nyingine Ridhiwani ameshiriki sherehe ya Miaka 10 ya Taasisi ya Ifm Charity kwa kufungua Vyoo vilivyojengwa na Taasisi hiyo katika kituo cha kulelea watoto Yatima cha Hope- Miono.
No comments:
Post a Comment