BILIONI 24.4 KUSAIDIA VIJANA WALIOATHIRIKA NA DAWA ZA KULEVYA NCHINI. - MAIPAC MEDIA TANZANIA

Breaking

MAIPAC MEDIA TANZANIA

A Centre for Indigenous and Pastoralists Community Informations




Sunday 25 June 2023

BILIONI 24.4 KUSAIDIA VIJANA WALIOATHIRIKA NA DAWA ZA KULEVYA NCHINI.

 

RAIS SAMIA SULUHU HASSANI akizungumza na wakazi wa Arusha katika siku ya kilele Cha kupinga madawa ya kulevya Nchini 



.Serikali yatangaza mkakati wa Kudhibiti biashara na Kilimo Cha bangi



Mwandishi wetu, Arusha 


maipacarusha20@gmail.com


Waziri wa nchi Ofisi ya Waziri mkuu bunge sera na uratibu   Jenista Mhagama amesema  katika mwaka wa fedha Rais Samia Suluhu Hassan ametenga shs  24.4  bilioni sawa na asilimia  100  kwa lengo la kuwasaidia vijana waliokuwa wanatumia madawa ya kulevya nchini .


Ameyasema  hayo leo katika maadhimisho ya siku ya kupiga Vita Dawa za kulevya madawa  


 Amesema ,pamoja na biashara ya dawa za kulevya  lengo kubwa ni kuhakikisha vijana wanakuwa salama na kuokolewa kutoka kwenye uraibu wa matumizi  wa dawa za kulevya.


 Mhagama amesema asilimia kubwa ya vijana ndiyo nguvu kazi ya Taifa katika kuleta maendeleo ndio maana serikali imeamua  kuwekeza nguvu kubwa katika kuwasaidia vijana kuweza kujikwamua katika changamoto  hiyo.


"serikali inatumia gharama kubwa kutibu watumiaji wa madawa ya kulevya na tayari mikakati ya kujenga kituo kikubwa cha madawa."amesema. 



Kwa upande wake Kamishna wa kuzuia na kupambana na madawa ya kulevya nchini Kamishna Jenerali Aretas  Lyimo amesema mpaka sasa wananchi  16 wamechukuliwa hatua kwa kujihusisha na ulimaji wa  zao la bangi mkoani Arusha.


Lyimo amesema elimu zaidi inaendelea kutolewa kwa wananchi katika kutambua madhara ya matumizi ya madawa hayo kwani yamekuwa yakiathiri afya za binadamu. 


"Tumekuwa tukitoa elimu kwa wananchi juu ya madhara ya dawa za kulevya kwani zimekuwa zikileta  athari kubwa kwenye ubongo  wa binadamu na tunataka  kuhakikisha  zao hilo linaisha  kabisa kwa jiji la Arusha na kwa watakaokaidi  watachukuliwa hatua kali za kisheria "amesema .



Aidha  ametoa wito kwa vijana waliotoka kwenye uraibu wa matumizi  ya  madawa ya kulevya na kuacha biashara ya madawa wana haki ya kuomba fedha katika mfuko wa halmashauri ili waweze kujiajiri pamoja na kuitaka jamii kuacha kuwanyanyapaa  vijana  wanaotumia madawa ya kulevya.



Kwa upande wa vijana waliotumia madawa ya kulevya wameiomba serikali pamoja na wadau kuweza kuboreshewa huduma kwa watumiaji wa madawa ya kulevya huku wakisema wamekuwa waelimisha Rika kwa jamii na kuwa mabalozi kwa jamii.



No comments: