MATUMIZI YA SHISHA KWA VIJANA KICHOCHEO KIKUBWA CHA MATUMIZI YA DAWA ZA KULEVYA NCHINI - MAIPAC MEDIA TANZANIA

Breaking

MAIPAC MEDIA TANZANIA

A Centre for Indigenous and Pastoralists Community Informations




Sunday 25 June 2023

MATUMIZI YA SHISHA KWA VIJANA KICHOCHEO KIKUBWA CHA MATUMIZI YA DAWA ZA KULEVYA NCHINI







NA: Mwandishi wetu


maipacarusha20@gmail.com

Ongezeko  la Matumizi ya Shisha nchini, limetajwa kuchochea matumizi ya dawa za kulevya nchini.


Vijana wengi wamekuwa wakijihusisha na kuvuta Shisha katika maeneo mbalimbali ya Burudani na starehe nchini.


Akizungumzia katika maadhimisho ya kitaifa ya siku ya kupiga Vita Dawa za kulevya Duniani Leo June 25,2023, Kamishna Jenerali wa Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya Aretas Lyimo amesema uvutaji wa Shisha umekuwa ukichanganywa na dawa za kulevya.


Lyimo amesema ,wamebaini baadhi ya wauzaji wa Shisha kuchanganya dawa za kulevya hatua ambayo imeongeza matumizi ya dawa za kulevya nchini.


"Matumizi ya Shisha yameongeza matumizi ya dawa za kulevya na kuchochea matumizi ya dawa hizo"amesema


Hata hivyo Kamishna Lyimo hakueleza hatua zaidi kuhusiana na uvutaji wa Shisha nchini.


Hata hivyo amesema, Mamlaka hiyo imejipanga Kupambana na dawa kulevya nchini hatua ambayo imefanya Tanzania Kuwa mfano wa Kudhibiti dawa hizo .


Amesema hata hivyo umefika wakati elimu juu ya athari za dawa za kulevya kutolewa kuanzia mashuleni ili Kudhibiti matumizi ya dawa za kulevya na biashara hiyo


Amesema Mamlaka hiyo inakusudia kujenga ofisi za Mamlaka hiyo katika mikoa kadhaa nchini ili kuimarisha Vita dhidi ya dawa za kulevya nchini.


Matumizi ya Shisha yaliwahi kuibua mjadala kutokana na aliyekuwa Mkuu wa Mkoa Dar es Salaam,Poul Makonda kuipinga marufuku.



No comments: