Erick Adam, enzi za Uhai wake |
Mwandishi wetu, Arusha
maipacarusha20@gmail.com
Jeshi la polisi mkoa Arusha, linamshikia msichana Brandina Fred kwa tuhuma za kumuuwa Mpangaji mwenzake Erick Adam, mkazi wa kijiji cha IIkirev ,Kata ya Olturoto wilayani Arumeru
Kamanda wa polisi mkoa Arusha, Justine Masejo amesema tukio hilo lilitokea majira ya mchana wakati, Blandina akiwa na kisu akijiandaa na kupika.
"Kilichotokea ni kuwa wote ni wapangaji walikuwa wakigombana huyu binti alikuwa na kisu kwa kuwa alikuwa jikoni, sasa ndio alimchoma mwenzake"amesema
Amesema Adam alifariki kutokana na kutokwa na damu nyingi b baada ya kuchomwa kisu.
Kamanda Masejo amesema, Jeshi hilo bado linamshikilia kwa mahojiano, mtuhumiwa huyo na bado anahojiwa kuhusiana na tuhuma hizo.
"Taratibu zikikamilika atafikishwa mahakamani kutokana na tuhuma ambazo zinamkabili" alisema kamanda Masejo
Mwili wa Adam umehifadhiwa katika hospitali ya rufaa ya Mountmeru kwa uchunguzi zaidi.
No comments:
Post a Comment