WAHITIMU WA MAFUNZO YA UKAMANDA NA UNADHIMU WATAKIWA KUTUMIA UJUZI WALIOPATA KULINDA AMANI AFRIKA - MAIPAC MEDIA TANZANIA

Breaking

MAIPAC MEDIA TANZANIA

A Centre for Indigenous and Pastoralists Community Informations




Wednesday 21 June 2023

WAHITIMU WA MAFUNZO YA UKAMANDA NA UNADHIMU WATAKIWA KUTUMIA UJUZI WALIOPATA KULINDA AMANI AFRIKA





NA: MWANDISHI WETU ARUSHA 

maipacarusha20@gmail.com


Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Innocent Bashungwa amewataka wahitimu wa  Mafunzo ya Kozi ya Ukamanda na Unadhimu kwenda kutumia ujuzi walioupata kusaidia ulinzi na amani katika nchi zao.


Maafisa wa jeshi 65  kutoka nchi 12 barani Afrika wakiwepo watanzania 49 walihimu mafunzo hayo katika mahafari yaliyofanyika juzi, katika chuo cha Ukamanda na Unadhimu, Duluti  wilayani Arumeru, mkoani Arusha.


Maafisa hao, licha ya kuhimu mafunzo hayo ya kijeshi pia,walihitimu shahada ya uzamili katika masuala ya ulinzi na usalama na baadhi astashahada  katika masuala ya ulinzi na usalama.


Akizungumza katika mahafari hayo ya kundi la 37/22-23, Waziri Bashungwa alisema kazi ya jeshi ni kazi ambayo imetukuka kutokana na kuwa na jukumu kubwa la ulinzi na usalama katika nchi.


Alisema anaimani wahitimu wa mafunzo, hayo watakwenda kuboresha utendaji wa kazi katika nchi zao na kuimarisha utendaji wa kazi na weledi katika masuala ya ulinzi na usalama.


“Mafunzo haya pia yanaimarisha mahusiano baina ya nchi mbali mbali katika masuala ya demokrasia  ya ulinzi na urafiki uliopo”alisema


Waziri Bashungwa aliwatunuku Wahitimu 65 Hadhi ya psc (Pass Staff College) na kuwakabidhi vyeti na zawadi kwa washindi waliofanya vizuri.


Awali, Mkuu wa Chuo cha Ukamanda na Unadhimu, Brigedia Jenerali Sylvester Damian Ghuliku, aliwapongeza Wahitimu na kuwatakia kila la heri wanaporejea kwenye vituo vyao vya kazi.


“Tunawahakikishia kuwa  Chuo kinaona fahari na kujivunia maarifa mliyopata mtakwenda kuyatumia vizuri katika nchi zenu na katika  vituo  vyenu vya kazi”alisema


Akitoa maelezo ya Kozi ya Ukamanda na Unadhimu, Kundi la 37/22-23, Mkufunzi Mkuu, Kanali Khaji Maulid Mtengela, alisema Wahitimu  wote wamefuzu na kufikia viwango vilivyowekwa, hivyo wanastahili kutunukiwa hadhi ya psc.


Wahitimu wa mafunzo hayo, walitoka nchi za Burundi, Malawi,Uganda, Uswatini,Afrika kusini,  Misri, Nigeria,Msumbiji, Rwanda,Kenya, Jamuhuri ya Kidemokrasia ya Congo na Wenyeji Tanzania.



No comments: